Facebook Comments Box

Wednesday, January 23, 2013

CHRIS BROWN NA RIHANNA WAKWARUZANA TENA


 
 Chris Brown na Rihanna ndani ya Swimming Pool
 
 

Nyumba ya Chris Brown iliyopo Holiwood Marekani

Polisi Hollywood Marekani wanamtafuta mwanaume ambae aliwafanya wakimbie spidi mpaka kwenye jumba la mwimbaji staa Chris Brown baada ya mwanaume huyo kuripoti habari za kutisha kwa alichoshuhudia nyumbani kwa Chris Brown.
Kwa mujibu wa CME, huyu mwanaume akijidai ni shuhuda alipiga simu kuomba msaada polisi baada ya kudai kashuhudia ugomvi wa mwanamke na mwanaume ukiendelea kwenye nyumba ya Chris Brown na baadae risasi zikapigwa baada ya majibizano ya mdomo kuzidi.

Kwa mujibu wa polisi ambao walikimbia spidi kuokoa hiyo hali kuendelea, hakuna chochote kilichotokea nyumbani kwa Chris Brown ambae hata hivyo hakuwepo nyumbani na wala hakuja tokea tukio kama hilo kwenye huo mtaa ndio maana kwa sasa wanachunguza ni nani alipiga simu na akawazingua kwa kuwapotezea muda na mafuta.

Huyu jamaa alikua anamaanisha ugomvi wa mwanamke na mwanaume yani ni Rihanna na Chris Brown ambao wanadaiwa kurudiana mapenzini sasa hivi baada ya kuachana kwa kesi ya Chris Brown kumpiga Rihanna kwenye penzi lao la mwanzo.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU