Facebook Comments Box

Sunday, November 4, 2012

LIVE SCORE : FT YANGA 2 - 0 AZAM, MTIBWA 2 - 0 SIMBA


Kutoka Taifa: Mpira umeisha Yanga wanatoka kifua mbele kwa Goli kwa sifuri

Kutoka Morogoro:  Mpira umeisha Mtibwa Inatoka kifua mbele kwa 2 kwa sifuri

Kutoka Morogoro: Gooooool Mtibwa wanapata goli la pili hapa. Nilisema huyu Javu ana historia ya kufunga katika uwanja huu. Ndio maana mara zote tunaandika mtibwa wanaongoza kwa goli la kwanza na hili ni la pili

Kutoka Mtibwa: Dk 88 Mtibwa bado wapo mbele kwa goli la kwanza

Kutoka Morogoro: Mwinyi kazimoto anaachia shuti kali linapanguliwa na kipa na kuwa kona. Simba wanalisakama lango la mtibwa

Kutoka Morogoro: Husein Javu anaingia kuchukua nafasi ya Muhamed Mkopi. Huyu Javu ana historia nzuri ya kufunga katika uwanja huu

Kutoka Morogoro: Dk 79 Okwi anawakosakosa mtibwa na inakuwa kona. Husein Sharrif anapewa kadi ya njano kwa kupoteza muda. askari wameongezwa uwanjani

 Kutoka Taifa: Gooooooool Yanga wanaongeza goli la pili. Ni Hamis Kiiza "diego" anafunga goli safi sana hapa. Alivua jezi hapa kiiza anapewa kadi ya njano

Kutoka Taifa: Abdi Kassim anachukua nafasi ya Hamis Mcha.

Kutoka Taifa: Msuva anaenda nje anaingia Luhende.Yanga wanakosa goli baada ya Kavumbagu kuchelewa krosi ya Niyonzima

Kutoka Taifa: Dk 51 Erasto Nyoni anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumkanyaga Niyonzima wa Yanga.

Kutoka Taifa: Dk 48 Bocco anashindwa kuuwahi mpira aliopigiwa na Khamis Mcha lakini Chuji anautoa na kuwa kona. Azam inapata kona ambayo inakolewa na mabeki wa Yanga.

Kutoka Taifa: Kipindi cha pili kinaanza hapa uwanja wa taifa kati ya Yanga na Azam

Kutoka Morogoro: Babu Ally anapewa kadi ya njano kwa kumfanyia madhambi emanuel Okwi. Na Mrisho Ngassa anaingia kuchukua nafasi ya Akuffor. Chollo anaingia nafasi ya Ochieng

Kutoka Morogoro: Mpira umeanza Jamal anatoka na anaingia Issa


Kutoka Morogoro: Washabiki wa Simba wamtupia chupa mwamuzi wa pambano hili, vile vile wamewarushia vilevile chupa wachezaji wao. mmoja wa washabiki hao wa simba amekamatwa na polisi. Ulinzi zaidi unahitajika katika mechi hii maana inaonekana washabiki wa simba hawana uvumilivu.

Taifa; Dk 45 HALF TIME..... AZAM 0-1 YANGA

 Kutoka Morogoro: Mtibwa wanapata kona tatu mfululizo, lakini, Kaseja anadaka, dakika ya 42 sasa

 Taifa: Dk 39 Yanga na Azam zinashambuliana kwa zamu na mpira unachezwa katikati sana.

Kutoka Morogoro: Mtibwa inaongoza kwa bao moja dhidi ya Simba, mfungaji Mohamed Mkopi. MTBWA 1-0 SIMBA


Taifa:  Dk 32 Azam inapata kona baada ya Mbuyu Twite kuutoa mpira nje
Khamis Mcha anapiga kona lakini Bocco anautoa mpira nje.
Dakika ya 28, Akuffor, anashindwa kutumia makosa ya mlinzi wa Mtibwa ambaye alipiga pasi fupi kwa mwenzake na kuiwahi. Lakini, akiwa ndani ya sita anashindwa kuamua kufunga au kutoa pasi, na kupiga pasi mkaa iliyonaswa na mlinzi wa Mtibwa. Dakika ya 30 sasa.
Kutoka Taifa: Dk 28 Bocco anapiga shuti kali langoni kwa Yanga lakini kipa Ally Mustapha anadaka
 Dk 26 Athuman Idd Chuji anamchezea faulo Michael Bolou.
Kutoka Morogoro: Kwa dakika 20 za mwanzo, mechi bado imebalansi hakuna mashambulizi ya maana sana ambayo timu zinayaandaa. Kila timu inacheza kama haitafuti ushindi. Mara mbili, mshambuliaji, Said Mkopi wa Mtibwa amejaribu kumtoka Amir Maftah, lakini hakufanya cha maana. Emmanuel Okwi anajitahidi kuwakimbiza mabeki wa Mtibwa Sugar, lakini bado hapati, sapoti ya karibu kutoka Sunzu na Akuffor. Mtibwa, wamepiga kona nne hadi sasa, wakati,Simba, wamepata kona moja tu. Kiujumla, mchezo bado umepooza hadi sasa.
 
 Kutoka taifa: Dk 18 Niyonzima wa Yanga,anakosa bao la wazi kwa kupiga nje mpira aliopokea kutoka kwa Oscar Joshua.
Dk 15 Erasto Nyoni wa Azam anamchezea rafu Msuva 
Dk 14 Simon Msuva wa Yanga anakosa bao la wazi baada ya kushindwa kuuwahi mpira uliopigwa na Haruna Niyonzima.
Dk 13 Mpira unachezwa kwa kasi sana na timu zote zinatawala kiungo
 
 Kutoka Morogoro - Kwa dakika hizi kumi za mwanzo, timu zote zinaonekana kucheza kwa kuogopana zaidi. Mtibwa, walianza kufika katika lango la Simba, kupitia kwa Shaaban Nditti. Walinzi wa Simba, Keita na Ochieng, wakamthibiti. Bado hakuna soka la kuvutia na la mipango, japo, Mtibwa, wanaonekana kucheza kitimu hadi sasa. Simba, wanapata kona ya kwanza, lakini haina madhara, dakika ya 12 
Dk 9 GOOO...... Didier Kavumbagu anaifungia Yanga bao la kwanza baada ya kutokea piga nikupige katika lango la Azam. AZAM 0-1 YANGA
Kutoka taifa: DK 3 Hamis Kiiza anakosa bao la wazi kwa upande wa Yanga.
 Kutoka taifa: Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya
Azam Fc Vs Young Africans
Morogoro - Mpira umeanza hapa Morogoro - Simba wakianza kwa kasi.
Leo tunaendeza utamaduni wetu wa kuwaletea matukio muhimu yanayoendelea kwenye viwanja tofauti vya ligi kuu ya Tanzania bara - kwa siku ya leo tunawaletea matukio ya mechi mbili kubwa kati ya Azam na Yanga, na Simba dhidi ya Mtibwa.
Kutoka Morogoro - Hiki ndio kikosi cha kwanza cha Simba kinachoanza: Kaseja, Kapombe, Maftah, Keita, Ochieng, Mkude, Kiemba, Kazimoto, Sunzu, Okwi, Akuffor
Hiki ndio kikosi cha Yanga ambacho tumefanikiwa kukipata. 
1.Ally Mustapha 'Barthez'
2.Mbuyu Twite
3.Oscar Joshua
4.Nadir Haroub 'Cannavaro'
5.Kelvin Yondani
6.Athuman Idd 'Chuji'
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo
9.Didier Kavumbagu
10.Hamis Kiiza
11.Haruna Niyonzima

Subs:
1.Yaw Berko
2.Juma Abdul
3.David Luhende
4.Nurdin Bakari
5.Nizar Khalfani
6.Jeryson Tegete
7.Said Bahanunzi


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU