Facebook Comments Box

Thursday, March 14, 2013

MOURINHO KURUDI CHELSEA? ABRAMOVICH AMPA BONGE LA ZAWADI

Mourinho na Abramovich
Tajiri wa Chelsea Abramovich amezidi kuimarisha uhusiano wake na Kocha wa Real Madrid Morinho baada ya kumnunulia zawadi ya saa yenye thamani ya fedha za kiingereza Paund 350,000 ambazo ni sawa na Dollar za kimarekani 400,000 ambazo ni sawa na fedha zetu za kitanzania Tsh 875,000,000 ( Milioni Mia nane na sabini na tano)

Kipindi cha Televisheni cha Kihispania kinachoitwa  Punto Pelota kimeripoti kuwa Morinho ataachana na Real Madrid mwisho wa msimu na kujiunga na Chelsea. Pia kituo hicho kimeripoti kuwa wachezaji wakongwe wa Chelsea wanajua kuwa viongozi wa kilabu hicho wanafanya mawasiliano na Morinho na atakuja kuchukua nafasi ya kocha aliopo sasa ambae ni Benitez.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU