Facebook Comments Box

Friday, August 5, 2016

WASANII WAWILI WALIOKUWA CHINI YA SHAROBARO RECORDS WAUAWA

 Ude Ude akiwa na swahiba wake Iqu Junior

Kitongoni Tanga
 
Taarifa kutoka tanga zinaripoti kuwa, wasanii wawili wa mziki wa Bongo fleva ambao walikuwa chini ya lebel ya Sharobaro records UDE UDE na IQU JUNIOR wameuliwa kwa risasi maeneo ya kiwanda cha cement cha Sungura Tanga kwa kosa la ujambazi ambapo walikuwa wanakimbizwa na Polisi.

Report ya Mkuu wa Polisi wa Tanga haijathibitisha tukio hili sio vibaya tukimjua Ude Ude ni nani kwani?,  Huyu alikuwa Msanii na muandishi mzuri wa mashairi ya mziki wa Bongo fleva na amekuwa akiwaandikia wanamuziki maarufu wa Bongo nyimbo ambazo huziimba kwa ufasaha.

Nyimbo alizowahi kuandika ni Single boy ya Ali Kiba, Wangu ya Lady Jaydee featuring Mr. Blue, Lofa ya Top C. Mbali na utunzi pia yeye Ude Ude ni mwanamziki kwani amewahi kutoa wimbo wake uitwao NGOMA INOGILE.

IQU ambae amefunga ndoa miezi michache tu, yeye ni mpiga picha na mwanamuziki pia aliishatoa wimbo aliomshirikisha Ali Kiba uitwao NISAMEHE.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU