Facebook Comments Box

Tuesday, October 21, 2014

KUHAMISHIA DALADALA KITUO CHA SIMU 2000 (NYUMA YA MAWASILIANO TOWERS) KUANZIA ALHAMIS TAREHE 23.10.2014

Baada ya kituo cha Simu 2000 kukamilika SUMATRA kwa kushirikiana na Manispaa ya Kinondoni na Kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Kinondoni tumekubaliana kufungua kituo hiki tarehe 23.10.2014 asubuhi, kwa daladala ambazo zilikuwa zinaishia au kuanza safari katika kituo cha daladala Ubungo.

Kila dereva anatakiwa kufuata utaratibu ulioelekezwa hapa chini ili kuondoa usumbufu usio na tija.

1. DALADALA ZINAZOTOKA MASAKI

zikifika barabara ya Shekilango zitaingia kulia kwa kutumia barabara ya TANESCO inayokwenda moja kwa moja kituoni simu 2000 na zitarudi barabara ya Shekilango kwa kutumia njia hiyo hiyo ya TANESCO.

2. DALADALA ZINAZOTOKA KARIAKOO, POSTA na KIVUKONI

zikifika mataa ya Ubungo zitaingia kulia (barabara ya Sam Nujoma) kwenda kituoni Simu 2000, zitarejea zilikotoka kwa kutumia barabara hiyo hiyo

3. DALADALA ZINAZOTOKEA BARABARA YA MANDELA

zitavuka mataa ya Ubungo (kwa kutumia barabara ya Sam Nujuma) na kwenda kituoni Simu 2000, zitarejea zilikotoka kwa kutumia barabara hiyo hiyo.

4. DALADALA ZINAZOTOKEA MWENGE

zikikaribia jengo la Mawasiliano Towers zitachepukia kushoto kwa kutumia service road inayopita mbele ya Mawasiliano Towers hadi kituoni simu 2000, zitarejea zilikotoka kwa kutumia barabara ya Sam Nujoma (sio servive road).

5. DALADALA ZINAZOTOKEA KIMARA NA MBEZI

zikifika mataa ya Ubungo zitaingia kushoto kwenda kituoni simu 2000. zitarejea zilikotoka kwa kutumia barabara hiyo hiyo.

Conrad Shio
Afisa Mfawidhi SUMATRA –DSM
0755 660 016


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU