Facebook Comments Box

Saturday, September 13, 2014

WENYE NYUMBA ZA KUPANGISHA KUANZA KULIPA KODI

Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) imesema ipo kwenye harakati za kuhakikisha wananchi wanalipa kodi kulingana na mfumo wa maisha yao.

Hayo yamesemwa na Meneja wa elimu ya Mlipa kodi kutoka kwenye mamlaka hiyo Diana Masala ambapo amesema kwa sasa TRA inafanya utafiti ili kufahamu ni jinsi gani ya kukusanya mapato kwa wananchi ambao wenye shughuli nyingi za kujiingizia kipato kikubwa kwa mwezi kupitia miradi midogo.

Amebainisha hayo katika semina iliyoandaliwa na walipa kodi pamoja na Mamlaka hiyo kuhusu ukusanywaji wa mapato na uendeshwaji wa ushuru wa forodha.

Ameeleza wapo wananchi wengi wenye nyumba zaidi ya moja na zenye wapangaji ikiwemo mifugo mbali mbali lakini ukiangalia kwa undani kwa mwezi zaidi ya kiasi cha shilingi 170,000/- zinakusanywa na wananchi hao, ambao baadae watatakiwa kulipa kodi.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU