Facebook Comments Box

Saturday, September 13, 2014

AZAM YAPANIA KUSHINDA MECHI YA KESHO



NI MECHI MUHIMU! Kocha mkuu wa klabu ya
Azam Joseph Marius Omog ameutaja mchezo
wa kesho wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga
kuwa ni mchezo muhimu. Omog amesema ni
muhimu kwa timu yake kushinda mchezo wa
kesho ili kuimarisha Morali ya timu kabla ya
kuanza kwa ligi. Azam inacheza mchezo huu
kwa mwaka wa tatu mtawalia ambapo miaka
miwili ya nyuma ilikua inacheza kama makamu
bingwa na mara zote ilipoteza dhidi ya
mabingwa Simba na Yanga, kesho inacheza
kama bingwa kwahiyo Azam ina nafasi kubwa
kushinda kama historia itatenda haki lakini pia
kutokana na maandalizi na usajili uliofanyika.
Raia huyo wa Cameroun alisema amewapa
wachezaji wake kilakitu kitakachowawezesha
kushinda mchezo huo, Kwahyo kazi imebaki
kwao kushinda na kuleta furaha klabuni.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU