Facebook Comments Box

Wednesday, August 27, 2014

YANGA YAIFUNIKA SIMBA ZANZIBAR

Timu ya Yanga  ya Dar es salaam  imewapoteza mbali mahasimu wao Simba katika  mapato  ya  mechi zao  za  kirafiki  zilizofanyika siku ya jumapili katika  uwanja wa Aman hapa Zanzibar.

Katika  mechi  hizo  zilizofanyika  jumapili  jioni  na usiku Yanga  iliteremka dimbani kupambana na Shangani fc  inayoshiriki  daraja la pili wilaya ya mjini hapa unguja na Simba ikapambana  na  Kilimani City  nayo pia  inashiriki katika daraja hilo hilo la pili wilya ya mjini, katika pambano la kwanza la Yanga liliofanyika majira ya saa  10 jioni liliingiza  shilingi mil 7.3, wakati lile la pili liloanza majira ya saa  2 usiku lilioihusisha timu ya Simba liliingiza  shilingi  mil 3.1 tu na kuzusha maswali mengi sana kwa wadau.
kwa kuwa pambano hilo lililofanyika  usiku na kuhudhuriwa na watu wengi  sana kuliko wale wa mchana,hali hiyo ilifanya  viongozi wa Simba wa mjini hapa wakiongozwa na Bw. Abdul Mshangama kuhoji kulikoni wao wapate mapato kiduchu namna hiyo na wakati  kwenye mechi yao ndiyo kulikuwa na watu wengi  na wamewatupia  lawama kuwa Kilimani  City  wamechakachua  mapato hayo.

Viongozi  wa  Mlimani walipatwa na kigugumizi na kuonyesha  kusikistishwa na hilo licha ya viongozi  hao  kuomba  radhi. Hali iliyosababisha hasira za viongozi wa Simba na kuwaambia wao walikuwa wamejenga urafiki lakini wameonyesha si waminifu katika pesa hizo  ndogo

"hizo  pesa ni ndogo na kusema kuwa kama wao Kilimani ndiyo waliomba na kuna makubaliano walikubaliana juu  ya usimamizi na mgawanyo wa mechi mapato hayo na hata kama watataka waje  Dar  tutacheza nao na hata  kama wanahitaji msaada  wa kipesa  tutawapa bila shida ila hawakutufurahisha kwa kweli" alisema kiongozi mmoja wa simba

Nayo  ZFA  wilaya ya mjini kupitia  katibu wake  Yahya  Juma  Ally  wameshngazwa na tukio hilo huku  wakiwatupia  lawama  viongozi hao wa Kilimani 

"kwa  kuwa waliwaambia viongozi wa  Kilimani City  walete  vitabu  vyote vya tiketi ili vigongwe  muhuri  wa  ZFA na baadae  sisi  tuje  kusimamia  hata  milangoni  lakini  wenzetu  walienda  kinyume wakaleta  vitabu  kidogo  tu  na hata  milangoni wakawa  wao  wenyewe bila kuishirikisha  ZFA" alisema kiongozi wa ZFA

Kwa hili lililotokea  ZFA  wilaya  mjini tumesikitishwa  sana na fedheha  hii  tuliyopewa na timu ya kilimani City na tutajitahidi lisitokee  tena kwenye mechi  zijazo aliongeza kiongozi huyo wa ZFA.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU