Facebook Comments Box

Thursday, April 10, 2014

HABARI YA KIUNGO WA ARSENAL ALIE JIUNGA NA JIHAD


Kiungo wa zamani wa Arsenal na Real Madrid
anayekipiga katika klabu ya Lokomotiv Moscow
Lassana Diarra amekanusha madai kwamba ni
mfuasi wa vita ya kidini nchini Syria.
Wiki iliyopita iliripotiwa kwamba Diarra (29)
alijiunga na vita inayoendelea Syria baada ya
kutolewa kwa video inayomuonyesha mtu akiwa
kajifunika uso huku akijitambulisha kwamba ni
Lassana Diarra.
Hata hivyo kiungo huyu wa timu ya taifa ya
Ufaransa ambae aliwahi pia kuitumikia
Portsmouth na Chelsea, ametoa taarifa rasmi
kupitia wakili wake na kusema hahusiki kabisa
na hiyo video.
“Hajawahi kukanyaga nchini Syria, yeye ni mwanasoka
anayeichezea Lokomotiv Moscow,” amesema
Mwanasheria wake.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU