Facebook Comments Box

Sunday, January 5, 2014

MAPINDUZI CUP: SIMBA WAVUTWA SHATI NA KCC



Wekundu wa Msimbazi Simba wameshindwa kuwatambia KCC ya Uganda baada ya kutoshana nguvu kwa kutoka sare ya bila kufungana katika mchezo wa kundi B kuwania Kombe la Mapinduzi uliochezwa uwanja wa Amaan usiku huu.
Kwa ujumla timu zote ziulionekana kucheza kwa umakini mkubwa hasa katika safu za ulinzi ikiwa ni ishara ya kuepuka kupoteza mchezo na kubakiza matumaini ya kufuzu kwa robo fainali. ambapo hadi mapumziko timu zote zilikuwa zimepiga mikwaju miwili tu iliyolenga lango la mpinzani.

Kipindi cha pili Simba ilionekana kuimarika zaidi hasa baada ya kuingia kwa Said Ndemla kuchukua nafasi ya Amri Kiemba na pia Betram Mwombeki aliyechukua nafasi ya Amissi Tambwe, ambaye alionekana kukosa ujanja wa kuipenya ngome ya waganda kwa kudhibiwa vilivyo. Kwa ujumla Simba walipiga mikwaju mingi zaidi iliyolenga lango kwani walipata mikwaju 6 wakati KCC walipiga mitatu

Simba Nusura waandike bao katika mwa kipindi chapili pale Ndemla alipopiga mkwaju mkali ambao hata hivyo uliokolewa na mlinda lango na ukawa kona butu.

KCC wangeweza kuandika goli la kusawazisha katika dakika za mwisho kabisa za mchezo kamasi uhodari wa mlinda lango Ivo Mapunda kuuucheza mpira uliokuwa ukielekea langoni na kufanya timu zote mbili zifune alama moja na kufikisha alama nne.

KCC iko kilelelni mwa kundi B ikiipiku Simba kwa wingi wa magoli ya kufunga wakati AFC na KMKM zinashika nafasi ya tatau na ya nne kwani zote zina alama moja kila moja. Michezo ya mwisho keshokutwa ndiyo itaamua ni tiu ipi iende robo fainali wakati Simba itakapocheza na KMKM na na KCC wakiikabili AFC Leopards

Kesho Jumamosi kuna michezo mine. Kwenye uwanja wa Gombani Pemba watoza ushuru wa Uganda, URA watapepetana na timu mseto ya Pemba (Clove Stars) kuanzia saa 8 mchana na baadaye saa 10 Mbeya CITY watakipiga na timu ya Chuoni.

Wakati hayo yakiwa Pemba, Unguja kwenye uwanja wa Amaan saa 10 jioni Ashanti United wataonyeshana kazi na timu mseto ya unguja (Spice Stars) na sa 2 usiku mabingwa watetezi Azam watawakabili Tusker ya Kenya.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU