Facebook Comments Box

Thursday, September 12, 2013

FAMILIA YA MATUMLA: TUNASHANGAZWA NA TAARIFA YA NDUGU ZETU KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA

TAARIFA za kukamatwa na unga kwa mabondia wawili Mbwana na Mkwinda wa familia maarufu ya mchezo wa ngumi nchini ya Matumla, zimeishangaza familia na jamii nzima ya Tanzania.

Bondia Rashid ‘Snake man’ Matumla ambaye ni kaka wa Mbwana na Mkwanda, amedai endapo itathibitika wadoeo zake wanajihusisha kusafirisha dawa za kulevya, watakuwa ameipa fedheha familia yao.

Mbwana Matumla ambaye ni mkubwa, ameelezwa kukamatwa mpakani mwa Uswisi na Ujerumani wakati Mkwanda Matumla amekamatwa Addis Ababa nchini Ethiopia.

Akikaririwa kuzungumza na wanahabari kadhaa, Rashid, bingwa wa zamani wa dunia wa WBU amesema:

    Tumesikia Mkwanda hadi ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia umethibitisha, lakini Mbwana bado hatuna uhakika ingawa hakuna anayeweza kumpata kwa sasa.

    Ni mwezi sasa umepita sina taarifa naye na hata wakati anaondoka hakuniaga, nimesikia kupitia

    vyombo vya habari. Kitendo cha mdogo wangu kukamatwa kimenisikitisha mno, siyo siri nimekwazika na ninarudia kusema hii ni fedheha kwenye familia yetu.
    
    Mimi mwenyewe nashangaa ni lini amejiingiza kwenye kazi hiyo, hata wakati anaondoka hakuniaga, mimi kaka yao na familia hatuelewi chochote.

    Unajua Mbwana hakumuaga hata mkewe, kweli inatusikitisha sana na tunasikia maumivu makubwa. Kama kweli itakuwa ni hivyo, basi watakuwa wameiangusha sana familia ambayo ilipigana kujenga jina. Lakini hatuwezi kuwatenga kwa kuwa ni ndugu zetu, tutawapigania.

Maisha:
Mkwanda alikuwa akiishi nchini Sweden ambako alikuwa na mpenzi wake aliyejaaliwa naye kupata mtoto mmoja aitwaye Liam aliyezaliwa mwaka 2010. Mpenzi wake huyo raia wa Sweden alikuwa mwanafunzi katika chuo kimoja mjini Norrkoping wakati Mkwanda alikuwa mwanafunzi katika chuo kingine akisomea Lugha ya Kiswidi. Alisema mdogo wake huyo alikuwa amebadilisha uraia na kuchukua uraia wa Sweden licha ya kwamba hapa Tanzania alikuwa amepanga Mbagala, Dar es Salaam na alikuwa anakuja na kukaa kwa muda na kisha kuondoka.

Kurejea:
Hivi karibuni inaelezwa alirejea jijini Dar es Salaam na alionekana ni mtu mwenye furaha na mishemishe kibao. Alikuwa anamiliki gari aina ya Toyota Vitz ambalo pia aliliuza lakini kuna taarifa kuwa, alinunua kiwanja katika moja ya maeneo ya Jiji la Dar.

Ngumi:
Katika familia ya Matumla, Mkwanda ndiye alikuwa bondia mdogo kuliko wote baada ya wengine sita. Kwa mujibu wa Rashid alipumzika kucheza ngumi miaka kadhaa iliyopita kutokana na kusumbuliwa na maradhi. Rekodi zinaonyesha kabla ya kupumzika kwa muda kucheza ngumi, Mkwanda alishinda mapambano manane (sita kwa KO) alipigwa mara tatu zote kwa KO alitoka sare mara moja tangu 2004. Mkubwa ni Ally ambaye ni marehemu, anafuatiwa na Rashid Matumla aliyewahi kuwa bingwa wa dunia mara mbili, bingwa wa mabara, Afrika mara moja na ndiye anaaminika kuwa bondia mkali zaidi ya wengine. Anafuatia Hassan, Mbwana ambaye anaelezwa ‘kudakwa’ Ulaya, Kareem na Mkwanda. 

--- Habari kwa mujibu wa magazeti ya MWANANCHI na GPL



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU