Facebook Comments Box

Thursday, September 12, 2013

JWTZ YAKANA TAARIFA YA JAMII FORUM, TWITTER NA FACEBOOK

JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO
Telex : 41051                                                      
Tele Fax  : 2153426
Barua pepe : ulinzimagazine@yahoo.co.uk
Tovuti : www.tpdf.mil.tz
Makao Makuu ya Jeshi,                
Simu ya Upepo  : “N G O M E”      
Simu ya Mdomo  : DSM  22150463
 Sanduku la Posta  9203,              
DAR ES SALAAM,                           

           12 Septemba, 2013. 
Taarifa kwa vyombo vya Habari

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) limepata habari kupitia mtandao wa Jamii Forumna Gumzo la Jiji  na mingineyo kuwa likizo zimesitishwa Jeshini  na waliokuwa  likizo wameitwa kurudi kazini.

          Taarifa hizo pia zimeeleza kwamba Brigedi za Tembo na Kifaru zimepewa maagizo ya kuwa katika hali 
ya utayari endapo watahitajika kusonga mbele.

          JWTZ  linapenda kuwaeleza wananchi pamoja na watumiaji wa mitandao hiyo kuwa taarifa hizo ni za upotoshaji mtupu na hazina ukweli wowote.  Aidha, taarifa hizo ni zenye nia ya kuzorotesha uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi yetu (Tanzania) na majirani zake. 

Sambamba na taarifa hii, pia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linapenda kutoa taarifa za kutohusika na viunganishi vya JWTZ kwenye mitandao ya  ‘Facebook‘ – (Facebook/JWTZ) na  ‘Twitter‘  (Twitter/ JWTZ).

Mitandao hiyo yenye viunganishi vya JWTZ imekuwa ikijihusisha na kutoa taarifa ambazo zimekuwa zikichangiwa na watu mbalimbali, ambapo baadhi yao wamekuwa wakitoa taarifa za upotoshaji  na zisizo sahihi.  Tunapenda kutaarifu kwamba akaunti za facebook na twitter zilizotajwa siyo za JWTZ.

Hatua zimechukuliwa za kuwatambua wahusika na kuwachukulia hatua za kisheria.

         Aidha inasisitizwa kwamba JWTZ lina taratibu za zake zinazotumika kufanya mawasiliano na Vyombo vya Habari, Taasisi, au mtu binafsi kuhusu utoaji wa taarifa.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi
Dar es salaam, Tanzania



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU