Meneja
 Msaidizi wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Mkoa wa Ilala, Catherine Nkelebe 
(kushoto), akizungumza na waandishi wa habari  Dar es Salaam jana , 
kuhusu  TRA mkoa huo kukamata bidhaa mbalimbali za dukani ambazo 
wafanyabiashara wanadaiwa kukwepa kuzilipia kodi kupitia mashine za 
kielektroniki.
 
Marobota ya bidhaa mbalimbali yakiwa TRA Mkoa wa Ilala baada ya kukamatwa.
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), 
Mkoa wa Ilala jijini Dar es Salaam, imekamata bidhaa mbalimbali za 
dukani zenye thamani ya mamilioni ya fedha ambazo wafanyabiashara 
wamefanya hujuma ya kukwepa kulipa kodi kupitia mashine za 
kielektroniki (EFD-Electronic Data Enterchange).
Meneja Msaidi wa TRA Ilala, 
Catherin Nkelebe akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es 
Salaam, alisema bidhaa hizo ambazo ni pamoja na sufuria, Khanga na 
mitumba zilikamatwa kufuatia msako unaoendeshwa na mamlaka hiyo kwa 
kushirikiana na Jeshi la Polisi.
Nkelebe alisema wafanyabishara 
wamekuwa wakitumia mbinu nyingi kuwepa kulipa kodi kwa kukataa kutumia 
mashine maalum za kielektroniki zilizotolewa na TRA kwa kukata 
stakabadhi kwa wateja wanaokwenda kununua bidhaa katika maduka yao.
Alisema ujanja unaofanywa na 
wafanyabiashara ni kwamba mteja akienda kununua bidhaa hususan katika 
maduka ya jumla wanampatia stakabadhi yenye thamani ndogo wakati mzigo 
huo unakuwa na thamani kubwa.
“Unakuta mfano mteja amenunua 
bidhaa za thamani ya shilingi milioni moja lakini mwenye duka anampatia 
stakabadhi mnunuaji yenye thamani ya Sh. 200,000 ili kukwepa kulipa 
kodi,”alisema.
Nkelebe alisema hujuma nyingine 
inayofanywa na wafanyabiashara ni kutoa stakabadhi ambazo hazina maelezo
 yeyote au mchanganuo wa bidhaa zilizonunuliwa kwa lengo la kuiibia 
serikali mapato yake.
Aliongeza kuwa wafanyabishara 
wanafanya ujanja huo kwa hofu ya kwamba iwapo wataandika stakabadhi 
yenye malipo halali watakadiliwa kiwango kikubwa cha kodi  wakati siyo 
kweli kwani TRA haifanya hivyo kwani inamkadiria mtu kodi kulingana na 
biashara yake.
Alisema TRA kwa kushirikiana na 
Jeshi la Polisi wataendelea kufanya msako wa wafanyabiashara wanaofanya 
hujuma hizo na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog