Facebook Comments Box

Friday, August 16, 2013

TRA ILALA YAKAMATA BIDHAA AMBAZO WAFANYABIASHARA WADAIWA KUKWEPA KODI KUPITIA MASHINE ZA EFD

2 
Meneja Msaidizi wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Mkoa wa Ilala, Catherine Nkelebe (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari  Dar es Salaam jana , kuhusu  TRA mkoa huo kukamata bidhaa mbalimbali za dukani ambazo wafanyabiashara wanadaiwa kukwepa kuzilipia kodi kupitia mashine za kielektroniki.
 
  3 
Marobota ya bidhaa mbalimbali yakiwa TRA Mkoa wa Ilala baada ya kukamatwa.


MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa Ilala jijini Dar es Salaam, imekamata bidhaa mbalimbali za dukani zenye thamani ya mamilioni ya fedha ambazo wafanyabiashara wamefanya hujuma ya kukwepa kulipa kodi kupitia mashine za kielektroniki (EFD-Electronic Data Enterchange).
 
Meneja Msaidi wa TRA Ilala, Catherin Nkelebe akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, alisema bidhaa hizo ambazo ni pamoja na sufuria, Khanga na mitumba zilikamatwa kufuatia msako unaoendeshwa na mamlaka hiyo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.
 
Nkelebe alisema wafanyabishara wamekuwa wakitumia mbinu nyingi kuwepa kulipa kodi kwa kukataa kutumia mashine maalum za kielektroniki zilizotolewa na TRA kwa kukata stakabadhi kwa wateja wanaokwenda kununua bidhaa katika maduka yao.
 
Alisema ujanja unaofanywa na wafanyabiashara ni kwamba mteja akienda kununua bidhaa hususan katika maduka ya jumla wanampatia stakabadhi yenye thamani ndogo wakati mzigo huo unakuwa na thamani kubwa.
 
“Unakuta mfano mteja amenunua bidhaa za thamani ya shilingi milioni moja lakini mwenye duka anampatia stakabadhi mnunuaji yenye thamani ya Sh. 200,000 ili kukwepa kulipa kodi,”alisema.
Nkelebe alisema hujuma nyingine inayofanywa na wafanyabiashara ni kutoa stakabadhi ambazo hazina maelezo yeyote au mchanganuo wa bidhaa zilizonunuliwa kwa lengo la kuiibia serikali mapato yake.
 
Aliongeza kuwa wafanyabishara wanafanya ujanja huo kwa hofu ya kwamba iwapo wataandika stakabadhi yenye malipo halali watakadiliwa kiwango kikubwa cha kodi  wakati siyo kweli kwani TRA haifanya hivyo kwani inamkadiria mtu kodi kulingana na biashara yake.
 
Alisema TRA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wataendelea kufanya msako wa wafanyabiashara wanaofanya hujuma hizo na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU