Facebook Comments Box

Saturday, March 16, 2013

KINANA NA UJUMBE WAKE WAKIWA MJI WA CHENGDU,CHINA


KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto) akimpa zawadi ya kinyago cha 'Ujamaa', Katibu Mkuu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC), Kamati Kuu jimbo la Sichuan, Zhang Ning, baada ya mazungumzo yao, Machi 15, 2013, katika hoteli ya Jinjiang, mjini Chendu, China. Kinana yupo nchini China  na ujumbe wa viongozi 14 wa CCM kwa ajili ya ziara ya mafunzo. (Picha na Bashir Nkoromo).

KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto) akipewa zawadi ya picha na Katibu Mkuu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC), Kamati Kuu jimbo la Sichuan, Zhang Ning, baada ya mazungumzo yao, Machi 15, 2013, katika hoteli ya Jinjiang, mjini Chendu, China. (Picha na Bashir Nkoromo

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (aliyefunfa mikono kifuani), na baadhi ya wajumbe katika msafara wake, wakimtazama kwa makini kijana, Hu Qingzhong, aliyekuwa akichora katuni kwenye kompyuta kwa ajili ya kuwekwa kwenye simu za mkononi. Kinana na ujumbe wake walipotembelea kituo cha Wajasriamali wasomi cha Chengdu-High-Tech zone, jijini Chengdu, China, Machi 15, 2013.  Kinana yupo nchini China  na ujumbe huo kwa ajili ya ziara ya mafunzo. (Picha na Bashir Nkoromo).
Katibu wa Jumuia ya Wanawake Tanzania (UWT) Amina Makilagi (kulia) akicheza muziki na mmoja wa wasanii wa kundi linalotumbuiza kwa kupewa fedha yoyote na anayevutiwa, kwenye eneo la Mji wa Kihitoria ya zaidi ya miaka 100 wa Jin Sha, jijini Chengdu, China.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU