Facebook Comments Box

Saturday, March 16, 2013

PAMOJA NA BARABARA KUKARABATIWA UPYA MAJI YAENDELEA KUTUAMA BUGURUNI SOKONI (BARABARA YA UHURU)

 Hii ni hali ilivyo sasa barabara ya uhuru baada ya barabara kukarabatiwa upya na lami iliyokuwepo kuondolewa na kuwekwa mpya. Kabla ya hapo maji yalikuwa yakituama na kusababisha eneo hili la barabara kuwa na mabonde na madimbwi mengi wananchi walipoona inakarabatiwa wakadhani kampuni iliyopewa kazi hiyo itazingatia hilo na maji hayatatuama tena. Cha kushangaza kwa mvua hizi ndogo maji yametuama tena kwa maana rahisi kampuni imechakachua kazi hii. Angalia picha hapo chini

Ukifika Rozana tu unaliona hilo dimbwi
Hili ni eneo la buguruni sokoni karibu na kituo cha polisi cha buguruni. Angalia maji hayo yalivyo tuama. Malaria haikubaliki? Kipindupindu je?
Kampuni imeshamaliza kazi hapo na lami mpya imewekwa


kwa mbaali unaliona dimbwi alilotengeneza bwana injinia

Ukiangalia vizuri utaona gari linavyowamwagia maji wapita njia pamoja na nyanya na matunda yanayowekwa hapo chini. Tunaolala hoi tunakazi sana

Matope yaliyocchanganyikana na uchafu wa sokoni buguruni.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU