Facebook Comments Box

Thursday, September 26, 2013

DAKITARI BANDIA ALIYEKAMATWA KCMC AFIKISHWA MAHAKAMANI MOSHI LEO



Daktari Feki Bw. Alex Sumni Massawe akipelekwa Mahakamani.

Mtu mmoja anayedaiwa kuwa ni daktari bandia aliyekamatwa akijiandaa kufanya upasuaji katika hospitali ya Rufaa ya Kcmc, leo atapandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi mjini Moshikusomewa shitaka lake kwa mara ya kwanza.

Mtuhumiwa huyo aliyetambulika kwa Jina la Alex Sumni Massawe alinaswa septemba 05, 2013 majira ya saa tano asubuhi ikidaiwa alitaka kumfanyia upasuaji mgonjwa aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa ngozi.

Mama mzazi wa kijana aliyetaka kufanyiwa upasuaji huo Bi Pamvelina Shirima alikutana na Daktari huyo katika Baa maarufu iliyopo eneo la Dar Street na kumtoza Shilingi 200,000/= akidai zitatumika kuharakisha mwanae afanyiwe vipimo vya upasuaji huo.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU