Facebook Comments Box

Thursday, September 26, 2013

BAADA YA KUONA WATAMKOSA MCHEZAJI KWA MSIMU MZIMA HATIMAYE YANGA WAMLIPIA NGASSA DENI LAKE KWA SIMBA

Mrisho Khalfan Ngassa akiwa katika Jezi tofauti za timu alizowahi kuchezea ambazo ni Simba, Azam na Yanga zote za Dar es Salaam.

Kikao cha mchana wa leo baina ya uongozi wa klabu ya Yanga ya Dar es Salaam na mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngassa kimefikia mwafaka kuhusu deni la mchezaji huyo kwa klabu ya Simba SC, Sh. Milioni 45, imefahamika.

Yanga SC italipa fedha hizo na Ngassa ataendelea kucheza katika klabu hiyo akiachana na mpango wa kwenda Oman, anakotakiwa na klabu moja ya huko, ambayo iko tayari kutoa kiasi cha Sh. Milioni 100, ambazo zingelipa deni la Wekundu wa Msimbazi na nyingine kulipwa Yanga ambao wana Mkataba naye kwa sasa.

Hata hivyo, haijajulikana Ngassa atailipaje fedha hizo Yanga, baada ya awali kuwapo kwa habari juu ya namna mbili, kwanza kukatwa mshahara na nyingine kuongezewa Mkataba.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU