Facebook Comments Box

Saturday, July 13, 2013

KIIZA ATUA LEO JIONI KUSAINI YANGA MIAKA MIWILI

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Friday Kiiza ‘Diego wa Kampala’ anatua Alasiri ya leo Dar es Salaam na ndege ya KQ tayari kusaini Mkataba wa kuendelea kuitumikia Yanga SC kwa miaka mingine miwili.  Hiyo inafuatia mpachika mabao huyo kufikia makubaliano na Yanga juu ya dau la usajili, baada ya awali kushindana hadi akarejea kwao, Kampala na ikaripotiwa alikuwa karibuni kusaini URA ya kwao. Mfanyabiashara mwenye jina mjini, Mussa Katabaro alikwea pipa hadi Uganda wiki mbili zilizopita kufanya mazungumzo ya kina na Kiiza ili abaki Yanga na hatimaye akakubali kuendelea kuvaa jezi za kijani na njano kwa miaka mingine miwili.
Anarudi; Hamisi Kiiza anatua leo
Katabaro ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga SC na mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya Mashindano, chini ya Mwenyekiti Abdallah Bin Kleb ameiambia BIN ZUBEIRY mchana huu kwamba Kiiza anatua na ndege ya shirika la Kenya, KQ Alasiri. Katabaro alipokuwa Kampala katika mazungumzo yake na Diego walikubaliana kumuongezea Mkataba wa miaka miwili kwa dau la dola za Kimarekani 40,000 na mshahara wa dola 1,500 kwa mwezi. Lakini Katabaro akaomba Kiiza akubali kuchukua dola 20,000 kwa sasa na dola 20,000 nyingine atampa katika mwanzo wa mwaka wa pili wa Mkataba wake. Kiiza akasema anataka dola 40,000 kamili kwa sababu ana kitu anataka kufanya na ndiyo maana alikataa kupokea dola 35,000 na gari, ilia pate fedha kamili. URA  ilikuwa tayari kumsaini Kiiza kwa mshahara wa dola 1,000 na dau la usajili dola 40,000 kama ambazo ameahidiwa Jangwani. Awali, Kiiza aligoma kusaini Yanga kutokana na kulazimishwa achukue dola 35,000 na dola 5,000 nyingine apewe gari.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU