Facebook Comments Box

Wednesday, May 29, 2013

UPDATES ZA KUHUSU MSIBA WA MANGWAIR IKIWEMO YA KUKATAZA NYIMBO ZAKE KUPIGWA CLOUDS FM

Picture
Pigo tena kwa muziki wa Bongo Fleva baada ya ripoti kusema, M To The P aliyekuwa na Mangwea jijini Johannesburg yupo hoi hospitali.


Mangwea na M To The P walisafiri pamoja hadi Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya onesho (show) na baadaye waliendelea na maisha, lakini jana  Mangwea alikutwa amefariki dunia chumbani na M To The P akiwa taabani na kulimbizwa hospitalini.


Picture
Picture
MIPANGO YA MAZISHI

Baba Mdogo wa Marehemu Mzee Mangwea ambaye yuko Mbinga, Songea kikazi, amesema kuwa wamekubaliana na kaka yake mkubwa (Baba mkubwa wa Ngwair), David Mangwea (ambaye naye yuko Songea) pamoja na kaka yao mwingine aliyepo Mara kuwa watu watakutanika Mbezi kwa msiba na mapokezi kutafanyika Mbezi Beach, Dar es Salaam.

Maziko ya mwili wa Ngwair yamepangwa kufanyika Morogoro sehemu ambayo baba yake pia alizikwa.

Kwa wakati huu, ndugu, jamaa na marafiki wa karibu wanawasiliana na Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini kuhusu namna ya kuleta miili ya marehemu hao nyumbani.

Taarifa zaidi zitatolewa kufuatana na maamuzi ya viikao vya familia.

Source: wavuti


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU