Facebook Comments Box

Wednesday, May 29, 2013

JIDE AAHIRISHA SHOO YAKE YA MIAKA 13 KUTOKANA NA KIFO CHA MSANII MWENZAKE ALBERT MANGWEA 'NGWEA'

Mwana Dada Komando katika mziki wa Bongo na mkongwe wa siku nyingi JUDITH WAMBURA 'Lady Jay Dee' Bint Machozi, Mamaa Somefood hayo yote ni majina yake si unajua tena sanaa, amesitisha onesho lake la kutimiza miaka 13 tangu aanze kufanya burudani lililokuwa lifanyike siku ya Ijumaa hii ya tar 31/05/2013 ndani ya Mjengo wake wa Nyumbani Lounge kutokana na Kifo cha Msanii mwenzake katika Bongo Fleva ambaye amepatwa na Msiba nje ya nchi huko Bondeni kwa MADIBA alikokwenda kutoa Show.
 
Jide amesema hayo alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha Super Mix kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha East Africa Radio kwa masikitiko makubwa sana, na amesema show hiyo haitafanyika kama ilivyokuwa imepangwa na badala yake mpaka tarehe nyingine itakapo pangwa tena.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU