Ambrose
 amesomewa  mashtaka 21 ya kuua na kujaribu kuua  wakati wa uzinduzi wa 
kanisa hilo ambao mgeni rasmi alikua Balozi wa Vatican nchini, Askofu 
Mkuu, Fransisco Padilla  ambaye alikuwa na mwenyeji wake Askofu Mkuu wa 
Jimbo Kuu la Arusha, Josephat Lebulu.
Katika 
hatua nyingine Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha,Liberatus Sabas amesema 
kuwa watuhumiwa watatu raia wa United Arab Emirates (UAE) Abdul Aziz 
Mubrak (30) ambaye ni mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato, Fouad Saleem 
Ahmed Hareez Al Mahri (29), Saeed Abdulla Saad (28) ambaye ni askari 
Polisi  na raia mmoja wa Saudia Arabia, Al Mahri Saeed Mohseens (29) wamekutwa hawahusiki na tukio hilo na wamekabidhiwa kwenye idara ya uhamiaji mkoani Arusha ili kuangalia kama waliingia kihalali nchini. 
Sabas amesema watuhumiwa wengine bado wanahojiwa kuona namna gani wanahusika na kitendo hicho cha kigaidi.
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
