Facebook Comments Box

Monday, April 1, 2013

WAKAZI WA BUKOBA WAMLAKI DIAMOND PLATNUMZ KWA KISHINDO













Jana msanii Naseeb Abdul aka Diamond Platnumz alitua mjini Bukoba, Kagera kuendelea na ziara yake ya kutumbuiza mikoa ya kaskazini magharibi. Kama inavyoonekana kwenye picha, umati mkubwa wa watu ulijitokeza kumlaki Diamond, kitu ambacho kilimpelekea msanii huyo kuchomoza juu ya gari kuwasalimia.

Kwa mujibu wa Diamond’s official website, kitendo cha Diamond kujichomoza juu ya gari kilisababisha msongamano mkubwa zaidi, na kusababisha barabara kufungwa, na baadhi ya kazi kusimama kwa muda.
“Juzi….Tarehe 30 march niliwasili salama salimini mjini bukoba Mkoani Kagera….Pili niwashukuru Mashabiki zangu wote Mkoani Humu kwa kunipokea kwa hali na mali ,Hii inaonyesha jinsi gani watanzania wanathamini na wana mapenzi na wasanii wao…..!!” aandika Diamond.

Aliongeza “Nililazimika kutoka Juu ya Gari kuwasalimu kabla sijaelekea hotelini…. Nilivotokeza hali ilizidi kuwa mbaya zaidi….Polisi walilazimika kufunga barabara kadhaa mjini bukoba na hata kazi zingine kusimama kwa muda kutokana na watu kuzingira Gari nilokuwepo kila kona nilipokuwa napita”. 
SOURCE:Diamond

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU