Facebook Comments Box

Friday, March 29, 2013

BREAKING NEWS: JENGO LA GHOROFA 16 LAPOROMOKA KATIKATI YA JIJI LEO HII


Taarifa iliyotufikia hivi punde inasema:
Jengo la ghorofa 16 limeporomoka asubuhi ya leo katikati ya Jiji la Dar es Salaam katika mtaa wa INDIRA GHAND karibu kabisa na Msikiti wa SHIA na Kuua watu watatu(3) na Kujeruhi kadhaa, ila inasemekana idadi ya watu wanao kadiriwa kuwa wamefunikwa na kifusi ni 60 lakini 17 kati yao tayari wameokolewa na kukimbizwa hospitali kwa ajili ya kupata matibabu.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda KOVA amesema Uokoaji unaendelea japo vifaa muhimu vya kuokolea bado havipo lakini wataalamu mbali mbali kutoka Manispaa wapo pale kuhakikisha hali inafanikiwa na kuwaokoa watu zaidi walioko ndani.


 Mtoto Maisamali Kareem (6) ambaye ameokolewa kutoka katika madrasa ya Msikiti wa Shia ulioangukiwa na Jengo hilo
 Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Kamanda Suleiman Kova na Kulia kwake ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala, Marietha Minangi.

 Kamanda Kova akizungumza na James Mbatia (Mbunge, Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi)


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU