Facebook Comments Box

Saturday, January 12, 2013

KIGOMA; NDEGE YA ATCL YAPASUKA KIOO IKIWA ANGANI

Hii ndio ndege ya kwanza iliyopata ajali Kigoma
 
ZAIDI ya abiria 25 waliokuwa wakisafiri na ndege ya Shirika la ndege nchini ATCL kutoka Kigoma kuelekea Dar es Salaam wamenusurika kifo kutokana na ndege waliyokuwa wakisafiria kupata hitilafu ikiwa angani jambo lililomlazimu rubani wa ndege hiyo kufanya jitihada na kuirudisha kiwanjani.

Hali hiyo imetokana na moja ya vioo vya mbele vya ndege hiyo kupasuaka na hivyo kuruhusu upepo mkali kuingia ndani na hivyo kuwafanya marubani wa ndege hiyo kufanya kazi ya ziada kuhakikisha ndege hiyo inatua salama.

Ndege hiyo ilikuwa ikifanya safari yake ya kwanza mkoani humo ikiwa ni miezi 10 baada ya ndege nyingine ya shirika hilo kuanguka na kuharibika mkoani Kigoma.

Baadhi ya abiria waliokuwemo kwennye ndege hiyo, Athumani Batumwa na Fred Mbassa wamesema ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 50, ilipata itilafu ya kioo cha mbele kiasi cha dakika 30 baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Kigoma.

Kaimu meneja wa shirila la ATCL, Kepteni Milton Lazaro amekiri kutokea kwa hitilafu hiyo na amewaondoa hofu wasafiri juu ta tatizo hilo nakwamba ni sehemu ya matatizo yanayoweza kutokea kwa ndege yoyote.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU