Facebook Comments Box

Monday, January 14, 2013

ANGALIA PICHA ZA MAANDAMANO YA WANAFUNZI WA IFM LEO


www.kitongoni.blogspot.com
Wanafunzi wa chuo cha usimamizi wa fedha wakiwa mbele ya geti la wizara ya ulinzi wakipeleka madai yao ya kuvamiwa na majambazi mara kwa mara. Wanafunzi hao walidai kuwa ijumaa walifanya kikao na jeshi la polisi cha ajabu kesho yake wanafunzi wawili walivamiwa na majambazi na kulawitiwa na kuibiwa vitu vyao.

Ulinzi ukiwa umeimarishwa wizarani kufuatia kadhia hiyo ya wanafunzi wa chuo cha usimamizi wa fedha
Hapa wanafunzi wakiwa safarini kwenda kumuona kamanda kova

Kamanda Kova akimsikiliza Rais wa wanafunzi wa Chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) akimuelezea kadhia nzima. Baadae Kamanda Kova aliamuru wanafunzi hao waende wote Kigamboni kushughulikia kadhia hiyo

Kamanda Kova akitoa taarifa kwa waandishi wa habari

Hapa wanafunzi wakiimba "tunavuka bure , tunavuka bure" huku wakielekea kwenye kivuko


Hapa wanafunzi wakigoma kushuka kwenye kivuko ilichukua saa zima ndio wakashuka na kuruhusu kivuko kiendelee na shughuli zake kama kawaida
Wakati wengine wakikataa kushuka wengine walikuwa wakiongezeka



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU