Facebook Comments Box

Monday, August 29, 2016

VITUO VIWILI VYA REDIO VYAFUNGIWA KWA MUDA USIO JULIKANA LEO



Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye amezifungia radio mbili kwa muda usiojulikana kwa makosa ya kuandaa vipindi ambavyo vimerushwa hewani vikiashiria uchochezi.

 Nape amesema kuwa uamuzi wa kuvifungia vituo hivyo umefikiwa baada ya kujirdhisha kuwa kipindi cha Matukio kilichorushwa Agosti 25, 2016 muda wa saa 2 usiku hadi saa 3 na Radio 5 pamoja na kipindi cha Morning Magic katika kipengele cha Kupaka Rangi Agosti 17 vilikuwa na maudhui ya uchochezi ambao ungeweza kuleta uvunjifu wa Amani.

Amesema kuwa kufuatia tukio hilo amevifungia viyuo hivyo kwa muda usiojulikana kwani wamekiuka masharti ya kanuni ya 5 (a,b,c na d), kanuni ya 6(2a, b na c) na kanuni ya 218 ya huduma za utangazaji ya mwaka 2005.








Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU