Facebook Comments Box

Wednesday, April 23, 2014

JE, HUU NDIO MWISHO WA WENGER ARSENAL?


Baada ya Manchester United kumfungashia virago kocha wao fununu,tetesi,masikio na macho yote yamehamia  kwa washika bunduki wa London

Wengi wanasema kuwa huu ndio mwisho wa enzi za mzee huyo hapo kilabuni

Baada ya Moyes kuachia ngazi,kocha
anayetajwa sana kurithi mikoba yake ni
boss wa timu ya taifa ya Uholanzi Luis
van Gal. 
Lakini Van
Gal amehusishwa kuhamia Arsenal na
gazeti moja maarufu la kwao uholanzi
liitwalo Vuetbal international state kwa
kutaja sababu kadhaa.

1:Wenger amebakiza wiki 6 tu katika
mkataba wake wa sasa na hajaongeza
bado.

2:Arsenal imemuajiri aliyekuwa msaidizi
wa Van Gal walipokuwa Bayern
Munich. Adries Jonker kama Director
of academy. (Mkurugenzi wa vipaji) hili likitafsiriwa kama
matayarisho ya ujio wa Van Gal.

3:Kama hilo halitoshi,Arsenal pia
imeshawaajiri makocha wadachi wa
vijana wa miaka chini ya 18 na 16 wanaoitwa Jans de kaart
na Luis van Hoon. Kitu
kinachotafsiriwa kwamba ni maandalizi
ya kumnyakua kocha mkuu mdachi.




Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU