Facebook Comments Box

Wednesday, September 17, 2014

KASEJA,DIDA,PONDAMALI NA BECHI LA UFUNDI LA YANGA WANA SIRI NZITO.



Hali  katika  klabu  ya  Yanga  kwa upande  wa  walinda  milango  inaonekana  si shwari, hali  hiyo  ilijionyesha  dhahiri  wakati  wa  mchezo  wa  ngao  ya  jamii  ambao  pia  ni  maalumu  kama  mchezo  wa  ufunguzi  wa  pazia ya ligi  kuu  ya  Tanzania  al  maarufu  Vodacom  Premier  Leagu (VPL).  wakati  timu  hiyo  ya wana  Jangwani  walikuwa  wakimbana  na timu ya waoka mikate  Azam  Fc   (wana  lamba lamba.)

Kilichowashtua  wengi  ni kule  kutokuwepo  kwa  ushirikiano  hata  kidogo kwa walinda  milango  hao  kabla  ya  mchezo huo  kuanza, kwa  kawaida  wakati  timu inayoanza  huwa  inachukuliwa  na  mwalimu  msaidizi  kwa ajili  ya  kuwapa  mazoezi  ya  kupasha  misuli  joto  makipa  huwa  wanakuwa  na  mwalimu  wao huku  akiwafanyisha  mazoezi  kabla  ya  mchezo, hivyo  ndivyo  hali  ndiyo  ilivyokuwa  kwa  upande  wa  Azam  wakati  wachezaji  waliokuwa  wanatarajiwa  kuanza  walikuwa  na  Trainer (mkufunzi) wao  Ibrahim  Shikanda  mchezaji  wao wa  zamani  wale  wa  akiba  wao  walikuwa  na  mwl  Kally  Ongara  akiwapasha joto  kwa  kufanya  nao  mazoezi  mepesi  mepesi, kwa  upande  wa  makipa  wao  walikuwa  na  mwalimu  wao  Idd  Abubakar  ‘Phantom’  aliyekuwa akiwafanyisha mazoezi  ya  kwa pamoja  huku  wakishirikiana  na  hata  walipomaliza  walikusanyika  wao  watatu  mwalimu  Idd  Abubakar, Mwadini  Ally  na  Ayishi  Manula  kwa  pamoja  wakaomba  dua  bila  kujali  nani  anaanza  katika  mchezo  huo  ndiyo  wakaenda  ndani  kwenye  vyumba  vyao  vya  kubadilishia  nguo.

Kwa  upande  wa  yanga  wao  wale  wanaonza  walikuwa  na  mwalimu  Salvatory  Edward  na Mwalimu  wao  Mbrazil  Leiva,wale  wasioaanza  kwenye mchezo  ule  wao  walikuwa  wakisimamiwa  na  mwalimu  Shedrack  Nsajigwa "FUSO" huku  wakifanya  mazoezi  mepesi. 

Kazi  ilikuwa  kwa  walinda mlango  wao sasa ndiyo  walioonekana  hawakuwa  na  ushirikiano  hata  kidogo  kuanzia  walipoingia,  Dida  alikuwa  mbele  ya  wachezaji  wakati  Kaseja  yeye  alikuwa  yuko  nyuma  ya  wachezaji  wengine  na  hakuna  sehemu  yoyote  ambayo  walishirikiana  hata  mmoja  kumpa  mwenzake  mpira  kitu  ambacho  si cha  kawaida  kwa  walinda  milango  na  aina  ya  mazoezi  wanayoyafanya  kabla  ya  kuanza kwa  mchezo hicho  ni  kitu  cha  kwanza.

Kitu cha pili, hata mwalimu wao Pondamali yeye  hakujishughulisha  na  kumuandaa  Kaseja  pia  kwa  ajili  ya  mchezo  huku  akijua  kwamba  hata  dakika  ya  10  tu  ya  mchezo  Dida  akiumia  atayeiingia  ni  Kaseja  ambaye  yeye  alikuwa  hajishughulishi  kabisa  na  kumuandaa  kimchezo  hali  ambayo  ilizusha  maswali  kwa wale  baadhi  tu  tuliogundua  kitu  hicho  na baadhi  yetu  tukawa  tunakwama  yupi  yuko  sahihi  kwa  kuwaandaa  makipa  kwa  kile  kilichokuwa  kinaendelea  pale  uwanjani  kati  ya  mwalimu  Pondamali   wa  Yanga  na  mwalimu  Idd  Abubakar  wa  Azam  bila  kupata  majibu.

 kitu  cha  tatu  na  cha  mwisho  ambacho  ni pale  Kaseja  alipojitenga  kabisa  na  Pondamali  na  Dida.
wakati  wao  wakiendelea  na  mazoezi  yeye  alikuwa  pembeni  kabisa  akicheza  ule  mchezo  maarufu  sana  dana  dana  huku  akifanya  manjonjo  ya  kuuchezea  mpira  peke  yake  mpaka  alipopata  msaidizi  na  yeye  kwa  kuwa  anapigiwa  mpira  na  mtu  wa  vifaa  wa  Yanga.

Hii  si  kawaida  kitimu  na  haijawahi  kutokea  kwenye  timu  yeyote  walipokuwa  pamoja  kuanzia  Simba  na  hata  Timu  ya  Taifa   Stars  na  hata  pale  Kaseja  alipokuwa  na  Ivo  Mpaunda  Timu  ya  taifa  haijawahi  kujitokeza  hali  ya  namna  hii  kiasi  cha  wadau  pia  kuona  kuwa  Pondamali  pia  ni  chanzo  cha  kuwagawa  makipa  hao  kwa  kuwa  yeye  kama  mwalimu  wao  haonyeshi  jitihada  za  kutaka  kuonyesha  kuwe  na  ushirikiano pale  wanapokuwa  kwenye  mechi  kama  ilivyokuwa  katika  mchezo  huo  wa  ngao. 

Ndiyo  maana  kitongoni  inahisi  kuwa  kuna  siri  nzito  ndani  ya  Yanga  inayowahusisha  Juma  Kaseja, Deo  Munishi  Dida, mwalimu  wao  Juma  Pondamali  Mensah  na  huenda  hata  Benchi  zima  la ufundi  chini  ya  Mbrazil  Maxio  Maximo  wanajua  nini  kinaendelea  katika  wawili  hao  na  jitihada  zetu  za  kuzitafuta  pande  zote  3 zinaendelea. 


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU