Hali 
katika  klabu  ya 
Yanga  kwa upande  wa 
walinda  milango  inaonekana 
si shwari, hali  hiyo  ilijionyesha 
dhahiri  wakati  wa 
mchezo  wa  ngao 
ya  jamii  ambao 
pia  ni  maalumu 
kama  mchezo  wa 
ufunguzi  wa  pazia ya ligi 
kuu  ya  Tanzania 
al  maarufu  Vodacom 
Premier  Leagu (VPL).  wakati 
timu  hiyo  ya wana 
Jangwani  walikuwa  wakimbana 
na timu ya waoka mikate  Azam  Fc  
(wana  lamba lamba.)
Kilichowashtua 
wengi  ni kule  kutokuwepo 
kwa  ushirikiano  hata 
kidogo kwa walinda  milango  hao 
kabla  ya  mchezo huo 
kuanza, kwa  kawaida  wakati 
timu inayoanza  huwa  inachukuliwa 
na  mwalimu  msaidizi 
kwa ajili  ya  kuwapa 
mazoezi  ya  kupasha 
misuli  joto  makipa 
huwa  wanakuwa  na 
mwalimu  wao huku  akiwafanyisha 
mazoezi  kabla  ya 
mchezo, hivyo  ndivyo 
hali  ndiyo  ilivyokuwa 
kwa  upande  wa 
Azam  wakati  wachezaji 
waliokuwa  wanatarajiwa  kuanza 
walikuwa  na  Trainer (mkufunzi) wao  Ibrahim 
Shikanda  mchezaji  wao wa 
zamani  wale  wa 
akiba  wao  walikuwa 
na  mwl  Kally 
Ongara  akiwapasha joto  kwa 
kufanya  nao  mazoezi 
mepesi  mepesi, kwa  upande 
wa  makipa  wao 
walikuwa  na  mwalimu 
wao  Idd  Abubakar 
‘Phantom’  aliyekuwa akiwafanyisha
mazoezi  ya  kwa pamoja 
huku  wakishirikiana  na 
hata  walipomaliza  walikusanyika 
wao  watatu  mwalimu 
Idd  Abubakar, Mwadini  Ally 
na  Ayishi  Manula 
kwa  pamoja  wakaomba 
dua  bila  kujali 
nani  anaanza  katika 
mchezo  huo  ndiyo 
wakaenda  ndani  kwenye 
vyumba  vyao  vya 
kubadilishia  nguo.
Kwa 
upande  wa  yanga 
wao  wale  wanaonza 
walikuwa  na  mwalimu 
Salvatory  Edward  na Mwalimu 
wao  Mbrazil 
Leiva,wale  wasioaanza  kwenye mchezo 
ule  wao  walikuwa 
wakisimamiwa  na  mwalimu 
Shedrack  Nsajigwa "FUSO" huku 
wakifanya  mazoezi  mepesi. 
Kazi ilikuwa kwa walinda mlango wao sasa ndiyo walioonekana hawakuwa na ushirikiano hata kidogo kuanzia walipoingia, Dida alikuwa mbele ya wachezaji wakati Kaseja yeye alikuwa yuko nyuma ya wachezaji wengine na hakuna sehemu yoyote ambayo walishirikiana hata mmoja kumpa mwenzake mpira kitu ambacho si cha kawaida kwa walinda milango na aina ya mazoezi wanayoyafanya kabla ya kuanza kwa mchezo hicho ni kitu cha kwanza.
Kitu cha pili, hata mwalimu wao Pondamali yeye hakujishughulisha na kumuandaa Kaseja pia kwa ajili ya mchezo huku akijua kwamba hata dakika ya 10 tu ya mchezo Dida akiumia atayeiingia ni Kaseja ambaye yeye alikuwa hajishughulishi kabisa na kumuandaa kimchezo hali ambayo ilizusha maswali kwa wale baadhi tu tuliogundua kitu hicho na baadhi yetu tukawa tunakwama yupi yuko sahihi kwa kuwaandaa makipa kwa kile kilichokuwa kinaendelea pale uwanjani kati ya mwalimu Pondamali wa Yanga na mwalimu Idd Abubakar wa Azam bila kupata majibu.
kitu cha tatu na cha mwisho ambacho ni pale Kaseja alipojitenga kabisa na Pondamali na Dida.
Kazi ilikuwa kwa walinda mlango wao sasa ndiyo walioonekana hawakuwa na ushirikiano hata kidogo kuanzia walipoingia, Dida alikuwa mbele ya wachezaji wakati Kaseja yeye alikuwa yuko nyuma ya wachezaji wengine na hakuna sehemu yoyote ambayo walishirikiana hata mmoja kumpa mwenzake mpira kitu ambacho si cha kawaida kwa walinda milango na aina ya mazoezi wanayoyafanya kabla ya kuanza kwa mchezo hicho ni kitu cha kwanza.
Kitu cha pili, hata mwalimu wao Pondamali yeye hakujishughulisha na kumuandaa Kaseja pia kwa ajili ya mchezo huku akijua kwamba hata dakika ya 10 tu ya mchezo Dida akiumia atayeiingia ni Kaseja ambaye yeye alikuwa hajishughulishi kabisa na kumuandaa kimchezo hali ambayo ilizusha maswali kwa wale baadhi tu tuliogundua kitu hicho na baadhi yetu tukawa tunakwama yupi yuko sahihi kwa kuwaandaa makipa kwa kile kilichokuwa kinaendelea pale uwanjani kati ya mwalimu Pondamali wa Yanga na mwalimu Idd Abubakar wa Azam bila kupata majibu.
kitu cha tatu na cha mwisho ambacho ni pale Kaseja alipojitenga kabisa na Pondamali na Dida.
wakati  wao  wakiendelea 
na  mazoezi  yeye 
alikuwa  pembeni  kabisa 
akicheza  ule  mchezo 
maarufu  sana  dana 
dana  huku  akifanya 
manjonjo  ya  kuuchezea 
mpira  peke  yake 
mpaka  alipopata  msaidizi 
na  yeye  kwa 
kuwa  anapigiwa  mpira 
na  mtu  wa 
vifaa  wa  Yanga.
Hii 
si  kawaida  kitimu 
na  haijawahi  kutokea 
kwenye  timu  yeyote 
walipokuwa  pamoja  kuanzia 
Simba  na  hata 
Timu  ya  Taifa   Stars 
na  hata  pale 
Kaseja  alipokuwa  na 
Ivo  Mpaunda  Timu 
ya  taifa  haijawahi 
kujitokeza  hali  ya 
namna  hii  kiasi 
cha  wadau  pia 
kuona  kuwa  Pondamali 
pia  ni  chanzo  cha  kuwagawa  makipa 
hao  kwa  kuwa 
yeye  kama  mwalimu 
wao  haonyeshi  jitihada 
za  kutaka  kuonyesha 
kuwe  na  ushirikiano pale  wanapokuwa 
kwenye  mechi  kama 
ilivyokuwa  katika  mchezo 
huo  wa  ngao. 
Ndiyo maana kitongoni inahisi kuwa kuna siri nzito ndani ya Yanga inayowahusisha Juma Kaseja, Deo Munishi Dida, mwalimu wao Juma Pondamali Mensah na huenda hata Benchi zima la ufundi chini ya Mbrazil Maxio Maximo wanajua nini kinaendelea katika wawili hao na jitihada zetu za kuzitafuta pande zote 3 zinaendelea.
Ndiyo maana kitongoni inahisi kuwa kuna siri nzito ndani ya Yanga inayowahusisha Juma Kaseja, Deo Munishi Dida, mwalimu wao Juma Pondamali Mensah na huenda hata Benchi zima la ufundi chini ya Mbrazil Maxio Maximo wanajua nini kinaendelea katika wawili hao na jitihada zetu za kuzitafuta pande zote 3 zinaendelea.
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog


