Facebook Comments Box

Wednesday, August 13, 2014

PICHA: MSIKITI WA MTAMBANI UNAUNGUA MOTO SASA HIVI

 

Juu ni picha mbalimbali zikionesha msikiti wa mtambani ukiungua moto. Hii ni sehemu ambayo hutumika katika harakati na kupigania haki waislam Tanzania. Chanzo cha moto huo bado hakijajulikana.
Hili ni pigo kubwa kwa waislam wa tanzania.

Inna lilahi wa inna ilayhi rajiuun.

Sekondari ya kiislam ya Mivumono (Mivuno Islamic Secondary) iliyopo
ndani ya msikiti wa Mtambani Kinondoni B, jijini Dar es Salaam.
Moto huo uliteketeza eneo lililokuwa likitumika kama mabweni ya
wanafunzi wa shule hiyo, maabara na ofisi za walimu, eneo hilo
limeteketea kabisa kiasi kwamba hakuna kilichoweza kuokolewa.
Chanzo cha moto huo kinadaiwa kusababishwa na hitilafu ya umeme
iliyokuwepo kwenye bweni la wasichana wanafunzi wa shule hiyo ila
hadi moto huo unafanikiwa kuzimwa hakuna mtu yeyote aliyepoteza
maisha wala kujeruhiwa.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU