Facebook Comments Box

Saturday, April 19, 2014

AZAM WATOA KIINGILIO MECHI YA LEO.


UONGOZI wa mabingwa wapya wa soka
Tanzania Bara, Azam FC unatarajia
kutowalipisha kiingilio mashabiki katika
mchezo wa kesho dhidi ya JKT Ruvu kwenye
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Katibu Mkuu wa timu hiyo, Nassor Idrissa
alisema sababu ya kufanya hivyo ni kuwapa
fursa mashabiki wao kuingia kwa wingi ili
kushuhudia timu yao ikikabidhiwa kombe la
ubingwa huo ambalo wanalitwaa kwa mara
ya kwanza tangu ilipopanda kucheza Ligi
Kuu.
“Natarajia kukutana na viongozi wenzangu
halafu tuzungumze na Mwenyekiti wa Bodi
ya Ligi, Silas Mwakibinga tuone kama
tunaweza kuruhusiwa kuwaingiza mashabiki
wetu bure kwenye mchezo wetu wa mwisho
dhidi ya JKT Ruvu, ili washuhudie timu yao
ikikabidhiwa kombe,” alisema Idrissa.
Idrissa alisema kama yangekuwa mamlaka
yao wenyewe na siyo sheria za Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF), wangechukua uamuzi
Ni


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU