Facebook Comments Box

Thursday, August 22, 2013

RAISI JAKAYA KIKWETE AFANYA MABADILIKO YA MAKATIBU WAKUU WA WIZARA MBALIMBALI


Katibu Mkuu Kiongozi, Mhe. Balozi Ombeni Y. Sefue akiongea  na Waandishi wa Habari waliojikusanya jioni hii kuhusu Uteuzi wa Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu Wapya, jijini Dar es Salaam. Pembeni kushoto ni Bw. Salvatore Rweyemamu, Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

Baadhi ya walioteuliwa:
Dr Florence Turuka - Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu
Bi Joyce Mapunjo -Katibu Mkuu wizara ya Afrika Mashariki
Bw Sihaba Mkinga -Katibu Mkuu -Habari, Michezo na Utamaduni
Bi Sofia Kaduma -Katibu Mkuu Kilimo na Ushirika
Dr Deo Mtasiwa -Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu akishughulikia Afya

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardh Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw Patrick Rutabanzibwa Amestaafu kwa hiari.
Wafuatao wameondolewa Ukatibu Mkuu na badala yake watapangiwa kazi nyingine:

1. Seth Kamuhanda
2. Kijakazi Mtengwa
3. Omary Chambo

Bw Peniel Lyimo aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu amehamishiwa Ofisi ya Rais kuwa Naibu Mtendaji Mkuu Kitengo cha PDU akishughulikia maswala ya Kilimo

  Orodha kamili ya walioteuliwa ni:
Jumanne Sagini amekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) awali alikuwa Naibu Katibu Ofisi wa Waziri Mkuu - TAMISEMI. Dk. Servacius Likwalile amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha,awali alikuwa Naibu Katibu.
Dk. Patrick Makungu- Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu katika wizara hiyo.

Alphayo Kitanda- Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, awali alikuwa Naibu Katibu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI. Dk. Shaaban Mwinjaka - Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi,awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, Dk.Uledi Mussa-Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, awali alikuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

Profesa Sifuni Mchome- Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, awali alikuwa Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania. Charles Pallangyo - Katibu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Anna Maembe -Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wizara hiyo, Sihaba Nkinga- Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo, Sophia Kaduma- Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

Naibu makatibu wakuu wapya walioteuliwa ni:
Angelina Madete- Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Regina Kikuli -Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Zuberi Sumataba -Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI anayeshughulikia suala la elimu, Edwin Kiliba -Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI.

Dk. Yamungu Kayandabila -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Adolf Mkenda -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha anayeshughulikia sera, Dorothy Mwanyika -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha anayeshughulikia Fedha za Nje na Madeni. Rose Shelukindo -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, 

Dk. Selassie Mayunga -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Monica Mwamunyange -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Consolata Mgimba -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Profesa Elisante ole Gabriel Laizer -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Armantius Msole -Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Waliopewa uhamisho kuwa ni:
John Mngondo amehamishiwa  Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia ametoka Wizara ya Uchukuzi, Selestine Gesimba - Wizara ya Maliasili na Utalii anatoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Injinia Ngosi Mwihava anahamia Wizara ya Nishati na Madini kutokea Ofisi ya Makamu wa Rais.

Maria Bilia -Wizara ya Viwanda na Biashara kutoka Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Nuru Milao anahamia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii.
Hiyo ndio orodha yote ya walioteiuliwa, kuhamishwa na kuacha kazi.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU