Facebook Comments Box

Friday, June 21, 2013

HIVI NDIVYO MIAMI HEAT WALIVYO CHUKUA UBINGWA WA NBA

Miami Heat Usiku wa jana Imefanikiwa Kutetea Ubingwa wake kwenye uwanja wa Nyumba AMERICAN AIRLINES ARENA kwa kuichapa Timu kongwe ya SAN ANTONIO SPURS kwa vikapu 95 kwa 88.

Alikuwa ni KING JAMES tena akiongoza Tim yake katika mbio hizi za mwisho za Ubingwa na kucheza katika kiwango bora sana usiku wa jana.KING JAMES aliipatia Timu yake vikapu 37 NA Rebounds 12 na kutoa assist za Kutosha kuhakikisha Ushindi unabaki nyumbani MIAMI,FLorida.Ikiwa ni kwa mara ya Pili Mfululizo MIAMI HEAT kuchukua kombe hilo baada ya mwaka Jana Kunyagua ubingwa Huo kwa Kuichapa Oklahoma City kwa game 4-2.Safari hii haikuwa Rahisi kwa HEAT kuchukua Ubingwa huo kwani Spurs walionyesha upinzani Mkubwa toka mwanzo wa Game 1,Fainali hii ilikuwa ya Piga nikupige Mpaka kufikia kufika katika Hatua ya GAME 7 ambayo ni kufa na kupona.HEAT kafanikiwa kuchukua Kombe hili baada ya ushindi wa Game 7.Wakitumia vizuri Mastar wao watatu(james,wade na bosh) Heat ilifanikiwa kupata ushindi huo.Ukiachana na Scores za King James,Wade pia alichangia Vikapu 23 NA rebounds 10,huku Bosh Akionekana kucheza Defence Nzuri Iliyo wapa shida sana Wachezaji wa SPURS.Wakizungumza na Vyombo vya Habari WADE na KING JAMES wameonekana ni watu wenye Furaha Huku wakishusha Sifa kemkem kwa wachezaji wa SPURS kwani haikuwa rahisi kwao Kuchukua Ubingwa huo kwa mara ya pili.HEAT imekuwa ni Timu ya Pili Kuchukua kombe hilo kwa mara ya pili Mfululizo kwa Miaka ya Karibu toka ichukue LA LAKERS 2009-2010.
Kwaa upande wa Spurs ambayo ndo Kwa mara ya kwanza Inapoteza Game Ya Fainali Katika Historia,Ilionekana Kuceza Vizuri kama kawaida Ila kila mtu akiwa na Mawazo na Majuto baada ya kupoteza Ushindi game 6 KATIKA hali isiyo tarajiwa,Akizungumza na Vyombo Vya habari Mmoja wa Wachezaji wakongwe wa SPURS MANU GINOBILI "Scientist" alisema bado akifumba macho anaiona GAME 6  gizanikitu ambacho wanajutia sana kupoteza mchezo Ule.Mkongwe timu Duncan katika harakati za Kutaka kuisaidia timu yake kuchukua Ubingwa Huo mara TANO akiwa na timu HIYO ziligonga mwamba jap alichangia vikapu 24 NA REBOUNDS 12.Alikuwa ni Kawhi Leornard Tena aliyekosa Mtupo Huru game 6 na kusababisha madhara kwenye timu Yake pia Game 7 ALIKOSA 3POINT ambayo ingeleta matokeo andapo angefunga na kuwaacha HEAT wakiambaa ambaa na ushindi.Tony Parker alikuwa kwenye kiwango chake lakini kazi Nzuri iliyofanywa na KING JAMES ya kumficha TONY parker asionekana kabisa kwenye game hiyo japo alipata nae Tab kidogo.DANNY GREEN aliyeonekana kung'aa zaidi game 5 Alipotea kabisa game 6 NA 7 NA KUWAACHA wakongwe wakiparangana.
HEAT imekuwa ndo timu ya Kwanza kuifunga Spurs kwenye Mchezo wa Fainali nd TIM DUNCAN,TONY PARKER,MANU GINOBILI ndo imekuwa mara yao ya kwanza Kupotea mchezo wa Fainali kwa fainali Tano walizoshiriki.Spurs Imeingia Fainali Za NBA mara TANO na imefanikiwa kuchukuwa mara NNE(1999,2003,2005,2007) na usiku wa jana kupoteza Huku HEAT IMEINGIA Fainali hizo mara mara NNE ikiwa Imechukuwa mara TATU (2006,2012,2013)Na 2011 ilipoteza Dhidi ya Dallas.

PICHA ZA MATUKIO YA GAME 7 KATI YA SPURS VS HEAT:

Tony Parker akijikuta kwenye wakati mgumu mbele ya KING JAMES Wakati akijaribu kuleta madhara.
VITA YA BOSH NA MKONGWE DUNCAN ILICHUKUWA NAFASI YAKE KAMA KAWAIDA MA'BIG HAWA WAKIKUTANA.
BOSH AKITIKISHA DEFENCE YA SPURS HUKU MONGWE MANU GINOBILI AKIHAKIKISHA ULINZI
KING JAMES LEBRON AKIFANYA YAKE MBELE YA WACHEZAJI WA SPURS KUDHIHIRISHA U'MVP WAKE.
FUNDI TONY PARKER AKIPIMANA UBAVU NA MARIO CHALMERS KUCHUKUWA BORI
MASHABIKI WA HEAT WAKISHANGILIA USHINDI WAO KWA KISHINDO IKIWA NI KWA MARA YA TATU SASA NA MARA YA PILI MFULULIZO.


MVP MARA NNE  na MVP MARA MBILI KWA SASA KING JAMES AKISUMBUA DEFENCE YA SPURS KUHAKIKISHA USHINDI UNABAKI NYUMBANI HUKU KAWHI LEORNARD AKIJARIBU KUMZUIA.



TIM "MKONGWE" DUNCAN AKIMTISHA TOTO CHRIS BOSH

TONY"FUNDI"PARKER AKIMCHAPA SHOOT MIKE MILLER.
MANU GINOBILI "SCIENTIST"AKIMPIGA FACE NORRIS COLE.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU