Facebook Comments Box

Thursday, April 11, 2013

UINGEREZA KUANZA KUTUMIA TEKNOLOJIA YA GOLI WEMBLEY


.
.
Timu zinazoshiriki ligi kuu ya England zinatarajiwa kukubaliana kupitisha matumizi ya teknolojia  ya mstari wa Goli maarufu kama GOAL LINE TECHNOLOGY baadaye wiki hii ambapo taarifa toka kwenye chama cha soka cha England imesema kuwa klabu hizo zimezungumzia suala la matumizi ya teknolojia hiyo na zitakutana tena siku ya alhamis ambapo agenda kuu ya mkutano huo inatarajiwa kuwa makubaliano ya kupitisha matumizi ya teknoljia hiyo kwenye michezo ya ligi kuu ya England kuanzia msimu ujao.
.
.
Kampuni ambazo zimeingia kwenye mashindano ya kuwania tenda ya ufungaji wa teknolojia hiyo kwenye viwanja vya ligi kuu ya England ni Kampuni ya HawkEye,Cairos,Goalcontrol na Goalref ambapo teknolojia hiyo itaanza kutumika kwenye mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu ya England ambao ni mchezo wa kuwania Ngao ya jamii unaochezwa kati ya mshindi wa ligi kuu na mshindi wa kombe la Fa, tayari shirikisho la mchezo wa soka ulimwenguni FIFA limepitisha matumizi  ya Goal line Technology ambapo teknolojia hiyo itaanza kutumika kwenye michuano ya kombe la mabara.
.
.
.
.
Chama cha soka cha England tayari kimepitisha matumizi ya teknolojia hiyo kwenye uwanja wake wa Taifa wa Wembley na kimeanza kupitia mapendekezo mbalimbali toka kwenye makampuni yanayofunga mifumo ya teknolojia hiyo.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU