Facebook Comments Box

Tuesday, December 17, 2013

SIMBA NA YANGA ZAPEWA JEZI KWA MPAMBANO WAO WA JUMAMOSI WA NANI MTANI JEMBE

KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager imekabidhi jezi kwa timu za Simba na Yanga kwa ajili ya mechi ya Nani Mtani Jembe itakayochezwa Jumamosi kuanzia saa kumi kamili jioni kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kampeni ya Nani Mtani Jembe  iliyozinduliwa Oktoba 6 mwaka huu itamalizika Jumamosi kwa klabu za Simba na Yanga kuchuana vikali pamoja na kuwania Sh milioni 100 zilizotengwa na Kilimanjaro Premium Lager ambao ni wadhamini wakuu wa timu hizo.


George Kavishe akiwakabidhi Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itangare na Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto jezi maalum zitakazotumika kwenye mechi ya Nani Mtani Jembe Jumamosi tarehe 21 Desemba. 


Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Meneja wa Kilimanjaro Premium Lager George Kavishe alisema wanakabidhi vifaa hivyo vyenye thamani ya Sh milioni 6.8 kwa ajili ya kuzipa mwonekano mpya timu hizo katika mechi hiyo.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Simba Joseph Itang’are ‘Mzee Kinesi’ aliwashukuru wadhamini hao Bia ya Kilimanjaro kwa vifaa hivyo huku akitamba timu yake kuibuka na ushindi.

Naye Ofisa Habari wa Yanga Baraka Kizuguto aliwashukuru wadhamini hao kwa kuwafanyia mambo mazuri na kuahidi kuendeleza mambo mazuri kwao na wataibuka na ushindi katika mechi hiyo.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU