Facebook Comments Box

Tuesday, December 17, 2013

RAISI KIKWETE AWATAKA WANANCHI KUWEKEZA KATIKA KILIMO ILI KUKUZA UCHUMI WA NCHI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Jakaya Mrisho Kikwete amesema endapo jamii itafanikiwa kuwekeza katika kilimo basi uchumi wa Tanzania utakuwa na kufanikiwa kupiga hatua katika maendeleo ya nchini.


Rais Kikwete ametoa msisitizo huo jijini Dar Es Salaam wakati wa mkutano wa saba wa baraza la Taifa la Biashara TNBC uliokutanisha taasisi binafsi na za umma kwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya taasisi hizo za pandembili.


Kilimo ni moja ya sekta ambayo imekuwa ikisisitizwa siku hadi siku, ingawa utekelezaji wake umekuwa ukisuasua katika baadhi ya jamii za kitanzania.
 
Miongoni mwa masuala yaliyozungumzwa katika mkutano huo uliotawaliwa na viongozi kutoka taasisi binafsi na umma ni pamoja na mpango wa Matokeo Makubwa sasa ambao unaonekana kufanikiwa zaidi kutokana na ushirikiano utakaokuwepo baina ya sekta hizo.

Mkutano huo pia umejadili changamoto mbalimbali ikiwemo suala la ajira kwa vijana na namna gani sekta binafsi inaweza kuimarishwa ili iweze kuzalisha ajira.
 
Viongozi mbalimbali wa serikali na taasisi binafsi akiwemo Waziri Mkuu Mizengo Pinda na mawaziri wa serikali wemehudhuria mkutano huo uliolenga kuimarisha ushirikiano baina ya taasisi binafsi na za umma.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa bodi ya Tanzania National Business Council muda mfupi kabla ya ufunguzi wa Mkutano wa TNBC uliofanyika katika hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaa.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU