Facebook Comments Box

Friday, November 1, 2013

MAZISHI YA LUTENI RAJAB MLIMA ALIYEUAWA CONGO YAFANYIKA KATIKA MAKABURI YA KISUTU

Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), wakiwa wameinamia kwa huzuni jeneza lenye mwili wa askari mwenzao, marehemu Luteni Rajab Mlima wakati wa maziko yaliyofanyika jana katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam jioni hii. Mlima ambaye alikuwa katika Jeshi la Umoja wa Mataifa la Kulinda Amani DRC Congo aliuawa akiwa kazini katika Mlima Gavana eneo la Goma.
Waombolezaji wakijiandaa kufanya maziko
Waombolezaji wakifanya maziko
Askari wa JWTZ wakitoa heshima wakati wa maziko
Meja Leonidas Luangisa akisoma wasifu wa marehemu Luteni Mlima.
Mseamaji Mkuu wa Familia ya Mlima, Balozi Alhaji Saleh Tambwe akisoma salamu za familia na kuwashukuru watu wote walioshiriki kwenye mazishi hayo.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU