Facebook Comments Box

Sunday, November 3, 2013

ANGETILE OSIAH APEWA LIKIZO YA LAZIMA NA RAIS MPYA WA TFF MPAKA MWISHO WA MKATABA WAKE

KIKAO cha kwanza cha Kamati mpya ya Utendaji ya Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF) jana chini ya Rais, Jamal Emil Malinzi kimemuengua
Katibu Mkuu wa kuajiriwa, Angetile Osiah Malabeja.
Rais Malinzi, alifungua kikao kwa ajenda ya kumuengua Angetile na
Wajumbe wakaafiki, lakini wanamng’oa kistaarabu.
Angetile amepewa likizo ya hadi atakapomaliza Mkataba wake mwezi
ujao na kwa sasa, aliyekuwa Ofisa Habari wa shirikisho hilo, Boniface
Wambura Mgoyo atakatimu nafasi yake.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
imemteua Bw. Boniface Wambura kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa TFF.
Uteuzi huo ni kuanzia Novemba 2 mwaka huu.
Aidha aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah ameagizwa aende
likizo ya malipo hadi atakapomaliza mkataba wake.
Kamati ya Utendaji inaviomba vilabu, vyama vya wilaya, vyama vya
mikoa, vyama shiriki na wadau wote kumpa ushirikiano Bw. Boniface
Wambura katika utekelezaji wa majukumu yake.
Jamal Malinzi
Rais, Dar es Salaam
Novemba 3, 2013



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU