Picha na Maktaba:
 
 
Matumizi ya dawa za kulevya nchini yamechukua sura mpya, baada 
ya kubainika kuwa watumiaji wengi wa dawa hizo aina ya heroin na cocaine
 sasa wanatumia dawa za hospitali zenye uwezo wa kulevya kuwa mbadala.
Watu wanadhani dawa za kulevya ni heroin na cocaine pekee, lakini
 vijana wanavuta petroli, gundi, dawa za maumivu na za kifua ambazo zina
 codeine, vyote hivi vinaathari,”    
Matumizi hayo mabaya yamebainika kutokana na 
kuwapo ongezeko la matumizi ya dawa za hospitali zilizo na nguvu 
inayoelezwa kulingana na dawa za kulevya zikiwamo heroin, cocaine na 
amphetamine.
Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Uhalifu na Dawa za 
Kulevya (UNODC) ya mwaka 2013, inathibitisha ongezeko hilo la matumizi 
ya dawa hizo, ambazo kitaalamu zinaitwa ‘new psychoactive substances 
(NPS).
“Dawa mbadala za dawa za kulevya zimezua wasiwasi 
mkubwa siyo kwa sababu ya ongezeko la matumizi yake, bali hata ukosefu 
wa utafiti wa kisayansi na uelewa wa matumizi yake,” ilisema sehemu ya 
ripoti ya UNODC.
Katibu Mkuu UNODC, Yury Ferdotov alieleza katika 
ripoti hiyo ya hali ya dawa za kulevya mwaka 2013 kwamba, changamoto 
kubwa iliyopo katika kudhibiti dawa hizo duniani ni matumizi ya dawa za 
hospitali na kemikali zinazotumika kuzitengeneza kutumika kama dawa za 
kulevya.
 Alisema nchi nyingi duniani hazina sheria wala 
uelewa kuhusu kemikali hizo, jambo linalosababisha wafanyabiashara 
wakubwa kuendelea kusafirisha kemikali hizo au kutumia teknolojia kulima
 mimea inayotumika kutengeneza dawa hizo.
UNODC limefafanua kuwa matumizi mabaya ya dawa 
hutokea wakati dawa za hospitali zinapotumika kwa malengo mengine 
kinyume na tiba.
Chanzo: Gazeti Mwananchi
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
