
WAZIRI Mkuu, 
Mizengo Pinda ameonja joto baada ya wananchi wa maeneo ya Mloganzira na 
Kwembe Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam kulala barabarani kama 
njia ya kushikiniza kutekelezewa madai yao. Pinda alikwenda Kwembe 
kutuliza mgogoro uliotokana na wananchi kudai fidia za viwanja vyao 
vilivyochukuliwa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya 
cha Muhimbili (MUHAS), ambapo majengo ya kisasa yanatarajiwa kujengwa 
katika eneo hilo. 
Chuo hicho kinatarajiwa kujengwa mpakani katika eneo hilo la mpakani 
kati ya Mlogazira (Pwani) na eneo la Kwembe lililopo Wilaya ya Kiondoni 
Mkoa wa Dar es Salaam. 
“Tuliweza kwenda Ofisi ya waziri ya ardhi na kupewa mchanganuo ambao 
ulikuwa unaeleza juu ya fidia ya ardhi na mazao yote yalipo juu ya 
mashamba na nyumba lakini wakati wa malipo tulikwazwa na malipo 
kiduchu,” alisema Chole. 
“Zoezi zima la ulipaji fidia katika eneo hili lilizungukwa na 
uchakachuaji katika ofisi ya Manispaa ya Kinondoni na MUHAS (Chuo cha 
Afya Muimbili),” alisema Chole. 
Naye Abasi Tamimu, alimtaka waziri mkuu kuangalia suala hilo kwa kina
 kwani wananchi wa maeneo hayo wamegeuzwa kafara katika mradi huo. 
Akijibu hoja hizo waziri mkuu Pinda, alisema kuwa Serikali imesikia 
kilio chao hivyo itaanza kulipa fidia kwa kuwalipa watu 93 ambao hapo 
awali walikuwa hawajalipwa. 
“Tutawalipa hawa wasiopewa chochote kwanza na nyie mliolipwa Serikali
 haiwezi kuwafidia mara mbili labda tuangalie utaratibu wakulifanyia 
kazi ombi lenu hilo la kupewa viwanja hivyo ngoja nikae na watendaji 
wangu kisha nitawaletea jibu,”alisema Pinda. 
Aliongeza kuwa katika hilo serikali itamua kutumia ubinadamu hili 
kuweza kupunguza matatizo ya wakazi hao na kuhahidi kushughulikia madai 
ya uchakachuzi wa fedha kwa wale wote wenye vielelezo. 
Hata hivyo wananchi hao waliridhishwa na majibu ya waziri mkuu, 
wakisema kuwa hawana jambo jingine zaidi ya kusibiri utekelezaji wa 
kauli ya Pinda kwa kuwa ni kiongizi wa juu serikalini. 
Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, 
Profesa Anna Tibaijuka, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana, 
na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick.
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog