Facebook Comments Box

Saturday, August 17, 2013

ABAKWA, ATOBOLEWA MACHO NA KUINGIZWA VITU SEHEMU ZA SIRI

Picture
Mwanamke mmoja anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 hadi 30 amekutwa amekufa katika makaburi ya Majengo katika soko la mjini Kahama mkoani Shinyanga huku mwili wake ukiwa ametobolewa macho na kuonesha kupigwa na kitu kizito usoni.

Mwanamke huyo ambaye hajatambulika jina lake wala anakotoka, alikuwa amevaa blauzi nyeusi yenye madoa meupe, viatu vyenye urembo wa rangi ya fedha, ni mnene kiasi, mweusi na mwenye nywele ndefu.

Mwili wa Mwanamke huyo amegunguliwa leo majira ya saa sita mchana baada ya watu waliokuwa wanachimba kaburi kuuona mwili huo pembeni ya eneo hilo na kutoa taarifa kwa Polisi.

Majirani wanaoishi eneo la makaburi hayo wanahisi unyama huo umefanyika usiku wa kuamkia jana huku, baadhi ya akina mama wakikiri kusikia sauti ya mwanamke akipiga yowe katika eneo la mnadani.

Jeshi la Polisi wilayani Kahama limethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku mrakibu msaidizi wa Polisi Aziz Mayunga akitoa wito kwa wananchi kufika katika chumba cha kuhifadhia maiti ili kuutambua mwili huo.

--- kitongoni blog haina ujasiri wa kuweka picha za marehemu ila kwa anayetaka kuziona tafadhali bofya  hapa uende mwenyewe kwenye chanzo cha taarifa hii blogu ya Bundala William Kijukuu cha Bibi "KJ" kuzitizama!


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU