Facebook Comments Box

Tuesday, May 7, 2013

TCU YAIFUNGIA KIU KUTOA SHAHADA YA UZAMILI NA SHAHADA YA UZAMIFU



 
Tume ya VyuoVikuu Tanzania (TCU) hivi punde imekitaka Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU) kusimamisha mara moja kufundisha au kutoa mafunzo ya Shahada ya Juu (Postgraduate), Shahada ya Uzamili (Masters) na Shahada za Uzamivu (PhD) katika kampasi ya Dar es Salaam, Tanzania.
KIU imeamriwa kusimamisha kutoa shahada hizo kuanzia LEO hawana wahadhiri wa kutosha wenye sifa stahili jambo ambalo ni kinyume cha taratibu.
Taarifa imetolewa na Katibu Mtendaji wa TCU, pia KIU imeamriwa kuzungumza na kushirikiana vizuri na wanafunzi wote waliodahiliwa katika kozi zilizotajwa hapo juu ili wahamie kwenye  vyuo  vingine vyenye  idhibati ya kutoa  mafunzo  hayo.
“Tume haitatambua shahada yeyote ya uzamili au uzamivu itakayotolewa na chuo hicho ambao watasoma katika kampasi ya Dar es Salaam, Tanzania.
“Chuo cha KIU Kampasi ya Dar es Salaam kina ithibati na kitaendelea kutoa mafunzo ya shahada ya kwanza (Bachelors), Diploma au vyeti zilizopitishwa na TCU kwa mujibu wa Ithibati husika tuu,” imesema sehemu ya taarifa iliotolewa na Katibu Mtendaji wa TCU.
Uamuzi huo umefikiwa  na tume hiyo katika mkutano wake wa hivi karibuni uliofanyika jijini Dar es Salaam.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU