Facebook Comments Box

Tuesday, May 7, 2013

RUGE HAJAJIBU SHUTUMA ZA LADY JAY DEE

 
Imewasilishwa na Jacob Buberwa --

Boss wa Clouds FM  Bw. Ruge Mutahaba katika maamuzi ya "hasira za mkizi" kashindwa kujibu shutuma za comando Lady Jay Dee

Wasanii amkeni kujua nani mchawi wa kazi zenu

Watanzania tulimsikiliza mkurugenzi wa utafiti wa redio Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba katika mahojiano na redio yake ya Clouds FM, mahojiano ambayo tulikua tukitegemea boss Ruge ajibu shutuma dhidi yake za kumtilia kauzibe katika kupata riziki mwanamuziki Lady Jay Dee bint machozi.

Katika mahojiano hayo ambayo sisi wasikilizaji tunayafananisha sawa na "Kesi ya Nyani na mwamuzi awe Ngedere", tulichokua tunakitegemea ni majibu ya shutuma lakini cha kushangaza Ruge kashindwa kabisa kujibu shutuma zinazomkabili, baadala yake akawa anarusha maneno na kuhusisha mifano ya wasanii walioshuka na kupanda.

Ruge alikwenda nje ya hoja ya msingi na mwisho wa mahojiano alikurupuka kwa kauli za kuamrisha kuwa ni maarufu kupiga nyimbo za kizazi kipya (Bongo Fleva) kwa muda wa siku nzima katika kituo cha Clouds FM.

Watanzania tunajiuliza, hivi redio ya Clouds FM au Redio ya Ruge na wasanii pamoja na sisi wananchi nani ni muhimu?

Kwa karne hii ambayo Taifa lina vituo vya redio zaidi ya 80?

Kwani wasanii wanamuhitaji sana Ruge na mshirika wake Bw. Kusaga, yaani wao ndiyo tuseme miungu ya wasanii?

Wananchi walio wengi wanamuunga mkono Lady Jay Dee kwa kutokukubali afanywe ngazi au kitendea kazi cha kuwanufaisha wanyonyaji katika soko la muziki, na kaamua kujitegemea. Maamuzi hayo ya Jay Dee ndiyo yanamfanya Jide atake kugeuzwa  "Kondoo wa Sadaka."

MRADI WA RUGE MUTAHABWA KATIKA SEKTA HII YA MUZIKI NI KUUA MUZIKI WA DANSI NA TAARABU NA KUJENGA MSINGI WA UTAMADUNI NA MZIKI WA KIZAZI KIPYA.

Ukisikiliza sana maelezo ya Ruge katika mahojiano utagundua wazi kuwa alijenga au alijaribu kujenga mtandao wa
kuwamiliki na kuwajenga wanamuziki wa kizazi kipya kwa manufaa yake, yaani mwanamuziki asipoingizwa katika
mtandao huu basi hatojulikana na kazi zake hazitotambulika.

Mtandao ambao pia unampendekeza msanii gani
akubalike kupewa tuzo hata kama si msanii mzuri.

Mtandao huu pia unatumika kama sururu la kuuchimbia kaburi
muziki wa dansi na muziki wa taarabu.

Mtandao huu pia unawalazimisha Watanzania walio wengi muziki gani wa kusikiliza, na mara nyingine kuwalazimisha wanamuziki nini cha kupiga (beat) n.k.

Leo Ruge anamsema Lady Jay Dee ampe kijiti mwingine. Lady Jay Dee alisema atapiga muziki kwa maisha yake na kuwaridhisha washabiki wake. Hakuna haja ya kupokezana vijiti katika gemu la muziki. Mfumo huu kupokezana vijiti ni mfumo unaoitwa "Ruge Mtahaba System" na wasananii wameshaushitukia kuwa si mfumo mzuri.

Je, wanamuziki wapo tayari kufanywa kete za kuchezea bao au chess?

Lazima wasanii wapate pumzi ya uhai kutoka katika mtandao wa Ruge?

Hivi wasanii hawezi kusimama kidete na kuungana kwa pamoja wakajipigania na kukataa kufanya wapagazi katika sekta hii?

Ruge kaonyesha kiburi kwa kusema muziki wa bongo flava usipigwe kwa siku nzima redioni Clouds, sasa wasanii na ninyi onyesheni mshikamano na msimamo wenu dhidi ya Ruge, kuwa nanyi ni muhimu kwa jamii ya Watanzania.

Je, nani mchawi wa kazi za wasanii na muziki wa Tanzania?

Watanzania na serikali ya Tanzania imeshuhudia kuangushwa kwa makusudi muziki wa dansi wa Tanzania na kuchimbiwa kaburi utamaduni na sanaa za maonyesho wa Watanzania, hujuma ambazo zinafanywa na mtandao ya siri ya wajanja wanaohujumu utamaduni na muziki wa Watanzania. Wanamtandao ambao wanaangaliwa macho bila ya kufanywa chochote na Watanzania au kuchukuliwa hatua zozote
na Serikali kupitia idara husika.

Leo Watanzania tunajiuliza, hivi hawa akina Ruge Mutahaba wanaijua historia, misingi ya
miziki ya Tanzania, na wale waliojitoa muhanga katika kujenga misingi hiyo imara? Mbona nchi za wenzetu
wanaendeleza misingi na miziki yao ya awali? Inakuwaje leo  baadhi ya wajanja wasiojua hata historia ya muziki wa Tanzania watuchagulia nini cha kusikiliza?

 "JOTO HASIRA"  KUNA HAJA YA KUWAFUKUZA KAZI NA KUVUNJA MTANDAO HUU UNAOHUJUMU UTAMADUNI, MUZIKI NA WASANII WATANZANIA!
 
SOURSE:WAVUTI


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU