Facebook Comments Box

Saturday, May 4, 2013

MH RAIS HOTUBA YAKO IMEACHA MASWALI MENGI KWA WANANCHI ULIO WAHUTUBIA

Dk.Shein-SMZ inawatambua walioshirikiana na Uamsho.

Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein amesema Serikali yake inawatambua watu walioshirikiana na Jumuiya ya Uamsho kuanzisha vurugu za kisiasa na kuacha kufanya kazi za kiroho kinyume na malengo ya kusajiliwa kwa jumuiya hiyo visiwani Zanzibar.

Dk Shein Akihutubia mkutano wa hadhara, Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja,  alisema jumuiya ya Uamsho iliwalazimisha polisi kutumia nguvu baada ya serikali kuwakanya na kuwaonya zaidi ya mara tatu wasitishe vurugu zao.

Alisema Serikali ina mikono mirefu na tayari imekwishawafahamu wote walioandaa mpango wa vurugu kwa kusingizia kero za Muuungano na wakati ukifika haitosita kuwachukulia hatua za kisheria ili kulinda amani na umoja wa kitaifa Zanzibar.

Alisema kifungu cha 19 (1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kimesema kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, wa imani na wa uchaguzi katika mambo ya dini pamoja na uhuru wa kubadilisha dini au imani yake bila ya kuingiliwa.

Alisema endapo yakizuka matatizo mengine yenye kutishia amani ya nchi Serikali yake itawatafuta wale wote waliohusika na kuwachukulia hatua za kisheria. 

Chanzo Cha Habari: Ipp Media.

 
 
 
 
 
 
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein amesema Serikali yake inawatambua watu walioshirikiana na Jumuiya ya Uamsho kuanzisha vurugu za kisiasa na kuacha kufanya kazi za kiroho kinyume na malengo ya kusajiliwa kwa jumuiya hiyo visiwani Zanzibar.

Dk Shein Akihutubia mkutano wa hadhara, Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja, alisema jumuiya ya Uamsho iliwalazimisha polisi kutumia nguvu baada ya serikali kuwakanya na kuwaonya zaidi ya mara tatu wasitishe vurugu zao.

Alisema Serikali ina mikono mirefu na tayari imekwishawafahamu wote walioandaa mpango wa vurugu kwa kusingizia kero za Muuungano na wakati ukifika haitosita kuwachukulia hatua za kisheria ili kulinda amani na umoja wa kitaifa Zanzibar.

Alisema kifungu cha 19 (1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kimesema kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, wa imani na wa uchaguzi katika mambo ya dini pamoja na uhuru wa kubadilisha dini au imani yake bila ya kuingiliwa.

Alisema endapo yakizuka matatizo mengine yenye kutishia amani ya nchi Serikali yake itawatafuta wale wote waliohusika na kuwachukulia hatua za kisheria. 
Kitongoni katika mahojiano yake na baadhi ya watu dhidi ya hotuba hiyo ya Mh Rais wengi walikuwa wanahoji kwanini serikali isiwakamate hao waliopanga vurugu au inasubiri mpaka vurugu zifanywe na watu wadhurike? Wengine walikuwa wakihoji uhuru wa kutoa maoni wa wananchi unaishia wapi? Kuna mambo wananchi hawapaswi kuyajadili?
Mwanasheria mmoja alieongea na Kitongoni yeye kwa maoni yake alisema Mh Rais anaiingilia uhuru wa mahakama kwa kuzungumzia mambo yaliyopo mahakamani na yakisubiri hukumu. "hotuba ya Mh Rais inaweza kumshawishi Hakimu au Jaji katika maamuzi yake."


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU