Facebook Comments Box

Monday, January 21, 2013

UKUTA WA STENDI YA UBUNGO WAANGUKA NA KUHARIBU VIBAYA MAGARI YA WATU LEO HII

 Ukuta wa eneo la ndani ya kituo cha Mabasi ya Ubungo Bus Terminal
 umeangukia magari zaid ya 19 (baadhi kama uonavyo pichani) zikiwemo
bajaji  tatu,yaliyokuwa yamepaki
eneo  ambalo hutumika kupaki  wakiwa wanasindikiza abiria na ndugu zao,aidha chanzo cha ajali hiyo kimeeleza
kuwa ni Mkandarasi wa eneo hilo aliyekuwa  akibomoa ukuta huo,na pia imeripotiwa
kuwa kuna baadhi ya majeruhi ambao wamekimbizwa hospitali kwa matibabu.


 Baadhi ya Maofisa kutoka Jeshi la Polisi wakiangalia baadhi ya magari yaliyoathiriwa vibaya mara baada ya kuangukiwa na ukuta mapema leo asubuhi kwenye eneo la kupaki magari,ndani ya kituo kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani.Ukuta huo ulikuwa ukibomolewa na Mkandarasi ikiwa ni hatua za awali wa kituo hicho kuvunjwa kwa ajili ya kupisha mradi wa ujenzi wa mabasi yaendayo kasi.


Si Magari tu,hata bajaji pia zimeathiriwa vibaya kama uonavyo pichani

Pichani juu ni baadhi ya magari mbalimbali yalioyoathiriwa vibaya kufuatia kungukiwa na ukuta.


Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, Afande Charles Kenyela akitoa maelekezo mafupi kwa baadhi ya maofisa wa Polisi waliokuwa wamefika kwenye eneo la tukio mapema leo asubuhi

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU