Facebook Comments Box

Tuesday, January 15, 2013

SUNZU AUZWA READING KWA BILLION 7 - AENDA KUFANYA VIPIMO VYA AFYA

Sentahafu wa Zambia Stopilla Sunzu amechukua likizo fupi kutoka kwenye kambi ya timu ya taifa kwa ajili ya michuano ya AFCON 2013 ili apate nafasi ya kwenda nchini England kwenda kufanya vipimo vya afya kwa ajili ya kujiunga na klabu hiyo. 

Sunzu ambaye anachezea klabu ya TP Mazembe ya DRC ambayo imeandika kwenye mtandao wake kwamba ada ya uhamisho ya $4.8million imeshakubaliwa na kilichobakia ni mchezaji kukamilisha vipimo vya afya. 

Mfungaji huyo wa penati ya ushindi ya Zambia dhidi ya Ivory Coast katika AFCON 2012, anatarajia kurudi Afrika ya kusini January 19, siku mbili kabla ya mabingwa watetezi kuchuana na Ethiopia katika mechi ya ufunguzi.

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU