Facebook Comments Box

Sunday, January 13, 2013

SAFARI YA YANGA YA MWAKA 1973 KUZINDUA TOTO AFRICA FC MWANZA ( Part II)

Waliosimama kuanzia kulia Mzee Kwala, Sululu, Chotta, Muhamed Mkweche, Muhamed Yahaya "Tostao" (anaechungulia jina lake halijapatikana) Kassim Manara,Shirsaz Shariff (wawili wa mwisho majina yao hayajapatikana) Waliochuchumaa kuanzia kushoto Abdulrahman, kibonge, Bilal Kabange, Muhamed Rishard Adolph, Muhamed Sengendo, Gordian Mapango, Jaffar Abdulrahman (wawili waliobaki majina yao hayajapatiakana ila kati ya hao wote ambao majina yao hayajapatikana mmoja wao ni Dr Ramadhan Dau)

Baada ya kuona ilivyopatikana timu ya Yanga B na mwaliko wa safari leo tunaendelea kuona safari ilivyokuwa na nini kilitokea.
Safari ilifanyika na ili kuwapa hamasa vijana Yanga ilitoa mchezaji mmoja kutoka timu ya wakubwa ambae alikuwa ni Boi Wiskens ambae alikuwa namba tatu mchezaji huyu alichezea hadi timu ya Taifa. Kutokana na ubovu wa barabara mchezaji wa Yanga B Muhamed Yahaya Tostao aliumia goti. walipofika wakakuta timu zitakazo shiriki ni Toto wenyewe kama wenyeji, Pamba na Cooperation United ya Shinyanga.Kikawaida list ya Yanga huwa inapangwa Dar Es Salaam ila Kocha Victor yeye alikuwa anaruhusu kipa kupanga beki yake na list ilikuwa hii ambayo ilicheza mechi ya kwanza na Pamba na kushinda 3 kwa 1.
1. Bilal Kabange 2. Jafar Abdulrahman 3. Shiraz Sharif 4. Muhamed Mkweche 5. Muhamed Rishard Adolph 6.Muhamed Yahaya Tostao 7 na 8 wamesahaulika 9 Kassim manara. Kipa alipomtaja Tostao kila mtu alikataa na kusema mgonjwa ila usiku wa walipofika Mzee Mangara Tabu Mangara alipiga simu hospitali ya mwanza (Bugando) na Tostao akapewa huduma na akaambiwa mechi ikiisha arudi kwa matibabu zaidi. Kama kawaidamechi zote Yanga walishinda kwa 3 kwa 1 isipokuwa moja tu Cooperation United ambayo walishinda 2 kwa 1 na golini alikaa Juma Pondamali messah. Baada ya mechi na kuchukua ubingwa Yanga walipewa zawadi ya saa ya ukutani kubwa ambayo walirudi na kuikabidhi kwa uongozi pamoja na kombe.
Baada ya kufika Dar Es Salaam Simba B waliomba barua ya kucheza na Yanga B kwenye uwanja wa Karume. Wakati huo Yanga B ikiwa haijafungwa mechi hata moja (watakubali au hawatakubali vipi iliundwa Nyota africa na Pan Africa Ijumaa ijayo itaendelea kwa ajili ya sehemu ya mwisho)

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU