Facebook Comments Box

Tuesday, December 18, 2012

BREAKING NEWS: MTU MMOJA AUWAWA KATIKA MAJIBIZANO YA RISASI KATI YA POLISI NA MAJAMBAZI KARIAKOO LEO HII

Mtu mmoja ameuwawa mida hii katika majibizano ya risasi yaliyotokea maeneo ya Msimbazi kariakoo, mtaa wa Livingstone kati ya Polisi na majambazi waliotaka kupora fedha zilizokuwa zinapelekwa benki ya NBC.

Majambazi hao waliokuwa wamevalia nguo za kiraia inasemekana walijua fedha hizo zinapelekwa leo hivyo walijiandaa kupora na Mapolisi nao waligundua hilo mapema hali iliyofanya majambazi hao kurusha risasi hovyo na kukimbia ili kukwepa kukamatwa.

Hadi sasa ni mtu mmoja anayeripotiwa kuuwawa ila bado haijajulikana kama ni raia au jambazi wale maana pia majambazi walivaa kiraia.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU