Facebook Comments Box

Monday, September 17, 2012

MWAKYEMBE AENDA KUINGIA MKATABA BERLIN

Waziri wa uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe na ujumbe wake wapo Berlin kuanzia tarehe 15 hadi 19 septemba kwa ziara ya kikazi. Moja ya tukio muhimu atakalo lifanya huko ni kusaini mkataba wa ushirikiano wa usafiri wa anga (Bilateral Air Service Agreement- BASA) baina ya nchi ya Tanzania na Berlin tarehe 17 septemba 2012. Tarehe 16 septemba Mheshimiwa alitembelea maonesho ya kimataifa ya sekta ya usafiri wa anga yaliyofanyika Berlin.
Mh Mwakyembe akiwa ndani ya moja ya ndege zilizokuwa kwenye maonesho hayo

Mh akipata maelezo kutoka kwa wataalam wa ndege za Airbus

Mh Mwakyembe akipiga picha na Balozi wa Tanzania Berlin Mh Ahmada (kushoto) na Afisa wa wizara ya uchuzi Ndg Ubwa (kulia)


Mh waziri akifanya mazungumzo na viongozi wa sekta ya anga wa Berlin



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU