Facebook Comments Box

Thursday, October 4, 2012

VODACOM WAZINDUA HUDUMA YA BIMA KWA NJIA YA SIMU

.
.
.
.
Taarifa kwa vyombo vya habari.
Watanzania sasa kupata Bima kupitia huduma ya M–Pesa.
  • Ni ushirikiano kati ya Vodacom na Heritage Tanzania kuzindua bima ya Faraja, Bima ya mazishi na ajali.
  • Wateja kununua na kulipia Bima kupitia M-Pesa.
  • Huduma ya bure kutolewa kwa wateja watakaolipia huduma mara kumi kwa Mwezi.
Dar-es salaam, Octoba 3, 2012 … Huduma ya Vodacom ya M-Pesa imezidi kupiga hatua baada ya kuwawezesha Watanzania kufanya malipo yao ya bima kupitia huduma hiyo.
Hii inafuatia ushirikiano kati ya Vodacom Tanzania na Heritage Tanzania kuzindua Bima ya Faraja, ambayo ni Bima ya mazishi ambayo inamuwezesha mlengwa kulipwa fedha taslim za mazishi kwa muhusika mwenye bima. Bidhaa mbalimbali ziko katika mpango huo ili kukidhi mahitaji ya wateja na bajeti ya malipo ya kila mwezi kuanzia shilingi 20000/= fadi 9800/= kwa Mwezi.
Mteja ana chaguo la kuongeza malipo kwa kuongeza huduma ya vifo vinavyotokana na ajali kulingana na faida na sera zao. Ongezeko hili la ziada litaongeza kiasi cha faida mara tatu kwa ongezeko dogo la malipo.
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Rene Meza, amesema wateja wa Vodacom wanaotumia M-Pesa, wataweza kujipatia bima ya bure kwa mwezi.
“Wateja wetu wote ambao watafanikiwa kutuma pesa walau mara 10 kwa Mwezi watapata  bima ya bure ya kiasi cha Shilingi laki mbili kwa mwezi unaofuata,” amesema Meza.
Suala la kipekee katika huduma hii ni kwamba hakuna haja ya kujaza fomu ili kujiunga na bima hii. Mteja atajiunga kwa njia rahisi kwa kupiga *150*00# na kuchagua kipengele cha bima. Vodacom inahakikisha kuwa wateja wote wa M-pesa wanaweza kupata huduma hii ili kuwa na amani ndani ya familia zao.
 “Ni muhimu kuthibitisha kuwa taarifa zako ni sahihi, na kuthibitisha kuwa unaelewa vigezo na masharti. Taarifa zako zitatumwa moja kwa moja kwenda Heritage Tanzania,” alisema Meza na kuongeza kuwa, “Unaweza kuchagua aina ya bima ambayo inakidhi mahitaji na bajeti yako,”
Bima hii ya Faraja pia itawawezesha kila mmoja kubadili au kuongeza kiwango chake kwa ile yenye faida zaidi kulingana na mahitaji yao na mabadiliko ya bajeti katika maisha yao.
Kwa taarifa zaidi kuhusiana na huduma mteja atapiga 0764 300001 bure au vipeperushi kutoka kwa wakala wa M-Pesa nchini.

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU