Facebook Comments Box

Tuesday, September 16, 2014

YAYA TOURE AINGIA UWANJANI NA BINTI ALIEVAA HIJJAB


Yaya Toure na Aisha
Aisha Dalal amekuwa msichana mdogo wa kwanza wa Kiingereza (Mascot) kuingia na wachezaji mpira Uwanjani akiwa amevaa Hijabu katika ligi kuu ya Nchini Uingereza.

Aisha aliyekuwa ameshikwa mkono na nyota wa mchezo huo Yaya Toure wakati wa kuingia uwanjani ilikuwa ni mechi baina ya timu za Manchester City na Liverpool iliyochezwa Agosti 26 mwaka huu. Matokeo ya mechi hiyo Man city walishinda 3-1.

"Ilikuwa ni kupata uzoefu kwangu na nilifurahia sana siku hiyo", alisema Aisha kuliambia Gazeti la Lancashire Telegraph.

"Wachezaji walikuwa marafiki mno kwetu na kutufanya tujisikie kama tupo nyumbani", alisema Aisha ambaye alikuwa na kaka yake mdogo aitwaye Khalil aliyeshikwa mkono na Samir Nasir wakati wa kuingia Uwanjani.
Aisha anasema walikuwa na bahati kwa kuwa waliruhusiwa kuchagua wachezaji waliotaka kuingia nao Uwanjani. 

Anasema kaka yake Khalil alichagua kuingia Uwanjani na Samir Nasri kwa kuwa ndiye mchezaji anayempenda na yeye alimchagua Yaya Toure.

Anaendelea kuhadithia Aisha kwamba Yaya Toure alikuwa mtu mzuri sana kwake kwani kabla ya kuingia alikuwa akimtoa woga kutokana na kelele kubwa za mashabiki.

Aisha anasema kuvaa kwake hijabu kulikuwa ni jambo muhimu sana na alijisikia ujasiri kufanya hivyo kwani hakuna aibu katika kudhihirisha imani yako popote pale ulipo.
 


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU